WIZARA YA MAJI KUIMARISHA TEKNOLOJIA KUDHIBITI UPOTEVU WA MAJI NCHINI

Date:

Share post:

Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, amesema Wizara yake itaendelea kuimarisha udhibiti wa upotevu wa maji katika mifumo ya usambazaji kwa kutumia teknolojia za kisasa katika mwaka wa fedha 2026/2027.

Akiwasilisha bajeti ya Wizara ya Maji, Aweso ameeleza kuwa hatua hiyo itahusisha matumizi ya mifumo ya usomaji mita kwa njia ya kielektroniki, ufuatiliaji wa mtandao wa maji (smart water management system), ukarabati wa miundombinu chakavu pamoja na ufungaji wa dira za maji za malipo kabla.

Alisema lengo la hatua hizo ni kuongeza ufanisi katika usambazaji wa maji na kupunguza upotevu unaotokana na hitilafu za kiufundi pamoja na matumizi yasiyo halali.

Aidha, Waziri Aweso amebainisha kuwa Wizara itaendelea kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya watu wanaojihusisha na uharibifu wa miundombinu ya maji na wizi wa maji, vitendo ambavyo vinachangia kwa kiasi kikubwa upotevu wa rasilimali hiyo muhimu.

Vilevile, amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kujenga uwezo wa wataalam wa sekta ya maji ili kuendana na mabadiliko ya teknolojia za kisasa, hatua itakayosaidia kuhakikisha usanifu wa miradi ya maji unakuwa imara na vifaa vinavyotumika vinakidhi viwango vinavyotakiwa kulingana na mahitaji ya miradi husika.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

BAHI YA TUMIA MICHEZO KUHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma imezindua kampeni maalum ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kupitia mashindano...

RC MAKALLA ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA UJENZI WA UWANJA NA BARABARA ZA AFCON ARUSHA

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Amos Gabriel Makalla amesema ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa uwanja wa michezo...

RUTO ATAJA UWEKEZAJI WA KENYA TANZANIA KUFIKIA DOLA BILIONI 1.7, AONYA URASIMU MIPAKANI

Rais wa William Ruto amesema kuwa takribani kampuni 500 kutoka Kenya zimewekeza jumla ya dola za Marekani bilioni...

RUTO ASISITIZA USHIRIKIANO WA EAC NI UFUNGUO WA KUKUZA BIASHARA NA AJIRA KWA WANANCHI

Rais wa William Ruto amesema nchi za Afrika Mashariki zina fursa kubwa ya kuongeza biashara ya ndani na...