MWENGE WAANGAZA MATUMAINI YA AJIRA KWA VIJANA MKURANGA

Date:

Share post:

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, Wazo Mwang’onda, amezindua mradi wa basi dogo unaoendeshwa na vijana wa kikundi cha UNAMA katika kijiji cha Picha ya Ndege, wilayani Mkuranga. Mradi huo unalenga kutoa huduma ya usafirishaji na kuongeza ajira kwa vijana.

Mwang’onda aliwapongeza vijana hao kwa kurejesha mkopo wao wa awali, hatua iliyowawezesha kupata nyongeza ya mtaji wa shilingi milioni 85.2 kupitia asilimia 10 ya mapato ya halmashauri. Alisisitiza kuwa mikopo hiyo ni muhimu kwa maendeleo ya vijana na taifa.

Naye Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, amesema mikopo hiyo imekuwa fursa ya kweli kwa vijana kujiajiri, huku akimpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kusimamia utekelezaji wake kupitia mapato ya ndani ya halmashauri.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya hiyo Bi.Khadija Nasir amesema Mwenge wa Uhuru 2026 umekagua miradi nane yenye thamani ya shilingi milioni 39.5 wilayani humo, ukiwemo miradi ya nishati safi, maji, elimu na viwanda, na utaendelea na mbio zake wilayani Kibiti.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

DKT MWIGULU AONGOZA KIKAO CHA MAWAZIRI WA BARA NA VISIWANI KUJADILI MUUNGANO

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba ameongoza Kikao cha Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na...

RAIS SAMIA AZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI BAHARI KUU JIJINI DAR ES SALAAM

Rais Samia amezindua meli hiyo leo Aprili 25,2026 kwenye ufukwe wa Makao Makuu ya Shirika la Uvuvi nchini...

TANAPA YAZIDI KUJIIMARISHA KIUTENDAJI, YAAPISHA MAKAMISHNA WAPYA WA UHIFADHI JIJINI DODOMA

Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) linaendelea kuimarisha mfumo wake wa uongozi na utendaji kazi kwa kuwapandisha...

JELA MIAKA 30 KWA KUPATIKANA NA BANGI

MAHAKAMA ya Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya imemhukumu Brown Frank Mwaitubi (31), mkazi wa Kajunjumele, kifungo cha miaka...