Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba ameongoza Kikao cha Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kilichojadili masuala ya Muungano. Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Golden Tulip, Uwanja wa Ndege-Zanzibar leo Aprili 25, 2026.
Kikao hicho pia kimehudhuriwa na Makatibu Wakuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.








