MAKAMU wa Rais na Mrithi wa Kiti cha Enzi cha Abu Dhabi, Sheikh Khalid bin Mohammed bin Zayed Al Nahyan, amewasili jijini Beijing nchini China kwa ajili ya kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na China.
Sheikh Khalid amepokelewa na viongozi waandamizi wa China, ambao walifanya mazungumzo ya awali yaliyojikita katika kukuza ushirikiano wa pande mbili, hasa katika sekta za biashara, uwekezaji na maendeleo ya uchumi.
Ziara hiyo inalenga kufungua fursa mpya za kiuchumi kwa mataifa hayo mawili, sambamba na kuongeza uwekezaji unaoendana na mabadiliko ya uchumi wa dunia na mwenendo wa masoko ya kimataifa.
Imeandaliwa na Razaki Mkuluma






