MHE. SILLO AWASILI JIJINI INSTANBUL – UTURUKI KUSHIRIKI MKUTANO WA IPU

Date:

Share post:

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Daniel Sillo (Mb) amewasili Jijini Istanbul, nchini Uturuki kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa 152 wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) utakaofanyika tarehe 15 hadi 19 Aprili, 2026.

Mhe. Sillo amewasili usiku wa kuamkia leo tarehe 13 Aprili 2026 kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Istanbul na kupokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Uturuki, Mhe. Iddi Seif Bakari, Naibu Mwakilishi wa Kudumu katika Umoja wa Mataifa, Uswisi, Balozi Dkt. Hoyce Temu na Mwakilishi wa Katibu wa Bunge la Tanzania kwenye Mkutano huo, Ndg. Daniel Eliufoo.

Mhe. Naibu Spika anaongoza Ujumbe wa Tanzania unaoshiriki Mkutano huo wa siku 5 akimwakilisha Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu.

Mkutano huo unatarajiwa kufunguliwa rasmi na Rais wa Uturuki, Mhe. Recep Tayyip Erdoğan na unawakutanisha Wabunge kutoka nchi 183 wanachama.

Mkutano huo pamoja na mambo mengine unatarajiwa kujadili masuala ya mazingira na hali ya ulinzi na usalama duniani na uchaguzi wa Katibu Mkuu wa Umoja huo.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...