Mwenge wa Uhuru umewasili Jijini Dar es Salaam leo tarehe 13 Aprili 2026, ukitokea Mkoa wa Kaskazini Unguja ambapo Mapokezi hayo yamefanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere – Terminal 1.
Mwenge wa Uhuru unaendelea na mbio zake za mwaka 2026, ambapo katika Mkoa wa Dar es Salaam unatarajiwa kukagua, kuzindua na kuweka mawe ya msingi katika miradi mbalimbali ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi.











