BEI ya mafuta duniani imeshuka baada ya Rais wa Marekani, Donald Trump, kukubali kusitisha mapigano kwa wiki mbili na Iran, hatua iliyoongeza matumaini ya kufunguliwa kwa Mlango-Bahari wa Hormuz.
Mlango huo muhimu hupitisha takriban asilimia 20 ya mafuta ya dunia, hivyo kufunguliwa kwake kunaweza kupunguza hofu ya upungufu wa nishati.
Bei ya mafuta ghafi ya Marekani imeshuka kwa zaidi ya asilimia 15 hadi chini ya dola 95 kwa pipa, huku Brent crude ikipungua kwa asilimia 13.75 hadi dola 94.68.
Hata hivyo, wachambuzi wanaonya kuwa bado haijawa wazi iwapo makubaliano hayo yatadumu au kama usafirishaji wa mafuta katika eneo hilo utarejea kawaida.







