WADAU WAITWA MAPAMBANO YA LISHE BORA

Date:

Share post:

MWANDISHI MAALUMU

WADAU wa lishe wameaswa kuunga mkono jitihada za serikali kupambana na changamoto za lishe wakati Tanzania ikijiandaa kufanya mkutano mkuu wa 11 wa wadau wa masuala ya lishe.

Rai hiyo imetolewa na jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe, Dk. Germana Leyna alipokuwa akihojiwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), jijini Dar es Salaam.

Dk. Leyna alisema Tanzania imepiga hatua kubwa katika kukabiliana na changamoto za lishe kwa sababu ya mikakati madhubuti iliyojiwekea.

“Serikali imeendelea kuweka mikakati mbalimabli ikiwemo kuendelea kutoa elimu kwa umma na kuhakikisha jamii inakuwa na uelewa wa masuala ya lishe ili kuendelea kuwa na taifa lenye watu wenye lishe bora.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe, Dk. Germana Leyna.

“Niseme hapa kuwa wadau waje tunganishe nguvu katika kupambana na changamoto za maswala ya Lishe,” alisema Dk Leyna.

Alisema serikali itahakikisha inawafikia wazalishaji hasa wakulima wawapo katika shughuli zao za kilimo ili kuwapa elimu ya lishe bora na umuhimu wa kutunza chakula kwa ajili ya matumizi ya nyumbani badala ya kuuza chote.

Dk. Leyna alisema wadau wanapaswa kuendelea kujitokeza na kuweka chachu katika masuala ya lishe nchini.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...