MSIMU WA MAUZO YA UFUTA KIDIJITALI WAFUNGULIWA

Date:

Share post:

ZERUBABEL CHUMA

MSIMU wa mauzo ya zao la ufuta kwa mfumo wa kidijitali umefunguliwa kuanzia April 25, 2025.

Taarifa kwa umma iliyotolewa leo na Mamlaka ya Udhibiti wa Mazao Mchanganyiko (COPRA), imeeleza kuwa utaratibu kwa wauzaji na wanunuzi wa zao hilo kwa msimu huu wa mauzo, utakuwa wa mfumo wa stakabadhi za ghala kwa kutumia minada ya kidijitali katika mikoa yote inayozalisha zao hilo.

Taarifa hiyo inawataka wananchi, wanunuzi na wadau wa kilimo kuzingatia maelekezo yaliyotolewa na serikali Januari 9, mwaka huu kuhusu orodha ya mazao ya kunde na mbegu za mafuta kuuzwa kwa mfumo wa stakabadhi za ghala na minada ya kidijitali kwa msimu wa 2024/2025.  

COPRA inawaonya wafanyabiashara wa mazao hayo kuwa hawaruhusiwi kununua mazao yaliyotajwa kupitia tangazo la serikali nje ya mfumo wa stakabadhi za ghala na kwamba ratiba za minada zitatolewa na COPRA yenyewe.

Aidha, COPRA inawarai wafanyabiashara kutojihusisha na ununuzi nje ya mfumo rasmi au kusafirisha mazao nje ya nchi bila vibali halali na au kughushi vibali kwani atakayegundulika kufanya vitendo hivyo atakuwa amekiuka sheria na hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.

Inazitaja hatua zitakazochukuliwa kuwa ni pamoja na kutaifisha mazao yatayogundulika kununuliwa au kusafirishwa kinyume na utaratibu, kuzuiwa kushiriki katika shughuli za ununuzi wa mazao ndani ya nchi, kutozwa faini pamoja na kufikishwa mahakamani kwa mujibu wa kifungu cha 22 cha sheria ya usalama wa chakula, sura ya 249.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...