NAIBU WAZIRI MAHUNDI KUFUNGUA BARAZA LA 42 LA UTAWALA LA UMOJA WA POSTA AFRIKA

Date:

Share post:

MWANDISHI WETU, WHMTH

Arusha 

NAIBU Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mkutano wa 42 wa Baraza la Utawala la Umoja wa Posta Afrika (PAPU), unaofanyika Makao Makuu ya Ofisi za Umoja huo, Jijini Arusha Juni 11 hadi 12, 2024.

Mhandisi Mahundi atafungua mkutano huo Juni 11, 2024 na utajadili maazimio na taarifa za vikao vya kamati za wataalamu wa masuala ya posta vilivyoanza Juni 3, 2024; vilivyojadili masuala mbalimbali yanayohusu fedha na utawala, mkakati, sera na kanuni, pamoja na uendeshaji na teknolojia.

Mkutano huu utahudhuriwa na wajumbe kutoka nchi wanachama wa PAPU pamoja na wadau mbalimbali wa Sekta ya Posta kutoka barani Afrika na wajumbe wa Sekretarieti ya Umoja wa Posta Duniani.

Baraza la Utawala la Umoja wa Posta Afrika ni jukwaa muhimu kwa maendeleo ya Sekta ya Posta barani Afrika, likiwa na jukumu la kuziunganisha nchi wanachama kupata fursa, kujadili changamoto na kutafuta suluhu endelevu kwa ajili ya kuboresha huduma za posta katika nchi wanachama 45.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...