SHAMBULIZI LA NDEGE ZISIZO NA RUBANI BAHARI NYEUS

Date:

Share post:

MOSCOW, URUSI

URUSI imeishutumu Ukraine kwa kufanya shambulizi “kubwa” la ndege zisizo na rubani kwenye makao makuu ya Meli zake katika Bahari Nyeusi mji wa bandari wa Crimea wa Sevastopol.

Shambulizi hilo lilianza saa 04:20 kwa saa za huko na kuhusisha ndege tisa zisizo na rubani na saba za baharini, maafisa wa Urusi walisema.

Takriban meli moja ya kivita inasemekana kuharibiwa katika mashambulizi hayo.

Hata hivyo, kraine bado haijathibitisha tukio hilo.

Mikhail Razvozhaev, gavana wa mji huo aliyewekwa na Urusi, alisema jeshi la wanamaji la Urusi limezuia shambulizi hilo.

Mashambulizi hayo ndio yalikuwa “makubwa zaidi” katika jiji hilo tangu Urusi ilipoanzisha uvamizi wa Ukraine mnamo Februari, vyombo vya habari vya serikali ya Urusi vilimnukuu gavana huyo akisema.

Alisema kuwa magari yote ya anga yasiyokuwa na rubani (UAV) yamedunguliwa na hakuna “miundombinu ya raia” iliyoharibiwa.

Meli moja imeharibiwa kidogo, Wizara ya Ulinzi ya Urusi ilisema.

BBC Swahili

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...