PRISONS YASUBIRI ‘MAAJABU YA SOKA’ KWA SIMBA

Date:

Share post:

KATIKA mchezo wa kesho Mei 10, 2026 dhidi ya Simba, Tanzania Prisons itahitaji maajabu ya soka tu ili kupata ushindi. Ni kwa mujibu wa takwimu za ‘Wajelajela’ hao msimu huu wa Ligi Kuu Bara.

Prisons ya jijini Mbeya haijaonja usindi katika mechi nane mfululizo za Ligi Kuu, na badala yake imefungwa sita na kuambulia sare mbili.

Kwamba mara ya mwisho kwa timu hiyo kupata pointi tatu za mchezo mmoja ilikuwa Februari 14, 2026, ambapo iliifunga Namungo mabao 3-2.

Katika mchezo wa kesho utakaochezwa katika Uwanja wa KMC, Mwenge jijini Dar es Salaam, watakutana na Wekundu wa Msimbazi, ambao hawajafungwa kwenye mechi 10 za Ligi za hivi karibuni (wameshinda sita na sare nne).

Aidha, katika mechi 10 za Ligi walizokutana na Simba hivi karibuni, Prisons wameshinda moja, wamepata sare moja na kufungwa mara nane.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

MLANGO-BAHARI WA HORMUZ UNAVYOITESA DUNIA

TEHRAN, Iran MGOGORO unaoendelea kati ya Iran na Marekani katika Mlango-Bahari wa Hormuz umetikisa uchumi wa dunia. Kila nchi,...

MWAKA MMOJA WA PAPA LEO AKIIONGOZA VATICAN

WASHINGTON DC, Marekani UMETIMIA mwaka mmoja tangu Papa Leo XIV alipochaguliwa kuliongoza Kanisa Katoliki duniani. Aliingia madarakani Mei 8,...

STEVE BARKER AMEANZA KUJIPATA LIGI KUU BARA

UKIFUATILIA msimamo wa Ligi Kuu Bara na kiwango cha Simba katika mechi za hivi karibuni, unaweza kusema sasa...

FEI TOTO KUVUNJA REKODI YA MIAKA MINNE LIGI KUU BARA?

TANGU George Mpole alipotwaa tuzo ya Mfungaji Bora Ligi Kuu Bara mwaka 2022, hakuna mchezaji mzawa aliyeweza kufanya...