SERIKALI KUSHIRIKIANA NA WADAU KUTOA ELIMU YA UPANDAJI MITI KWA BIASHARA YA KABONI

Date:

Share post:

Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeendelea kufanya jitihada mbalimbali ili kuhakikisha elimu ya upandaji miti inatolewa kwa wanachi hususan wale wa vijijini ili waweze kushiriki vizuri katika biashara ya kaboni.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Dkt. Festo Dugange wakati akijibu maswali kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais bungeni jijini Dodoma leo Aprili 30, 2026.

Katika swali lake Mbunge wa Viti Maalumu Mhe. Maryam Azan Mwinyi alitaka kujua Serikali ina mkakati gani wa kutoa elimu ya upandaji miti ili wananchi hasa wale wa vijijini washiriki katika biashara ya kaboni.

Akijibu swali hilo, Dkt. Dugange amefafanua kuwa Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na TAMISEMI, Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) imeendelea kutekeleza kampeni za upandaji miti katika halmashauri zote nchini, huku akiongeza kuwa vimeratibiwa vipindi vya redio na televisheni ikiwemo kipindi cha “Mazingira yetu na Tanzania Tuitakayo” kinachorushwa kila Jumatatu kupitia TBC ambapo elimu ya upandaji miti na biashara ya kaboni hutolewa.

Sambamba na hayo Dkt. Dugange ametumia nafasi hiyo kutoa rai kwa TFS kila kanda kusambaza miche kwa wananchi kwa ajili ya kuipanda katika maeneo yao na kuitunza, hatua itakayosaidia uhifadhi wa mazingira kuwa endelevu.

Hatahivyo Dkt. Dugange ameeleza kuwa Ofisi ya Makamu wa Rais inaendelea kuwajengea uwezo maafisa mazingira katika ngazi ya Serikali za Mitaa kuhusu umuhimu wa upandaji miti na fursa ya biashara ya kaboni ili kuhakikisha wananchi wote wanashiriki katika biashara hiyo.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

RAIS DKT. MWINYI APOKEA RIPOTI YA CAG ZANZIBAR YA MWAKA 2024/2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameipokea Ripoti ya Mdhibiti...

SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR KUENDELEZA USHIRIKIANO NA IRELAND

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Zanzibar itaendelea kuimarisha...

KAMBI YA WAKIMBIZI NDUTA KUFUNGWA KUFUATIA UREJESHWAJI WA HIARI WA WAKIMBIZI BURUNDI

Kambi ya Wakimbizi ya Nduta iliyopo Wilaya ya Kibondo, Mkoa wa Kigoma inatarajiwa kufungwa rasmi Leo Aprili 30,...

INTANETI YA KASI YAFIKIA ASILIMIA 94 MAENEO YA MAKAZI WATUMIAJI WAKIFIKA ASILIMIA 85.3

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Angellah Kairuki, amesema huduma ya intaneti ya kasi imefikia asilimia 94...