OKWI AIBUKA USAJILI MPYA SIMBA

Date:

Share post:

MSHAMBULIAJI wa zamani wa timu ya Simba, Mganda Emmanuel Okwi, amemuibua beki wa kikosi hicho, Fikiri Magoso, baada ya kumtaja katika usajili wa wachezaji wapya kwa ajili ya msimu ujao.

Magoso ambaye alikuwa kwenye kilichocheza fainali ya Kombe la Washindi Barani Afrika dhidi ya Stella Abdjan ya Ivory Coast mwaka 1993, alisema Simba wanatakiwa kufanya usajili wa wachezaji watano wa kigeni, akiwamo mshambuliaji mwenye kiwango cha juu kama alivyokuwa nyota wao wa zamani Okwi.

Magoso alisema pamoja na timu yao kufika fainali katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika msimu uliomalizika hivi karibuni, lakini kikosi chao kilikuwa na mapungufu mengi.
Beki huyo wa zamani wa Simba alisema uongozi wa klabu hiyo unatakiwa kusajili nyota wapya wa kigeni katika idara ya ushambuliaji, kiungo na mabeki ili waweze kufanya vizuri msimu ujao.

Alisema hakuridhishwa na viwango vya wachezaji wa kigeni waliosajiliwa msimu uliopita, hasa idara ya ushambuliaji, kwa kuwa hawakuonyesha ubora wao.

Magoso alisema anahitaji kuona anasajiliwa ushambuliaji mkali ambaye akitengenezewa nafasi mbili anafunga moja.

Alisema msimu uliopita walimkosa mshambuliaji mwenye uchu wa kufunga mabao kama aliyokuwa Okwi, kwani timu ilionekana kitengeneza nafasi nyingi lakini tatizo lilikuwa umaliziaji.

Katika msimu uliopita wa Ligi Kuu Bara, Simba ilishika nafasi ya pili, watani wao wa jadi Yanga wakitwaa ubingwq kwa mara ya nne mfululizo.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...

ISHU YA RASHFORD BADO PASUA KICHWA

MANCHESTER, UingerezaKOCHA wa Manchester United, Michael Carrick, amesema bado haijafahamika kama Marcus Rashford atarudi klabuni hapo au atabaki...

BARCA YAPATA MRITHI WA LEWANDOWSKI

CATALUNYA, HispaniaKLABU ya Barcelona imeanza mipango ya kumsajili mshambuliaji wa kati wa Real Mallorca, Vedat Muriqi, ikiamini anatosha...

ARSENAL AKILI YOTE KWA MONGA

LONDON, UingerezaARSENAL ya Kaskazini mwa Jiji la London imeonesha nia ya kumsajili winga anayefanya vizuri Ligi Daraja la...