ENDELEENI KUFICHUA UKATILI KWA WATOTO

Date:

Share post:

RIPOTA PANORAMA

WAKATI taasisi ya Save the Children, ikizindua dawati la ulinzi wa mtoto Shule ya Msingi Levolosi jijini Arusha na mabaraza ya watoto kwa lengo kupata taarifa za ukatili wanazofanyiwa watoto, vyombo vya habari vimeaswa kuendelea kufichua maovu wanayofanyiwa watoto, ili kuisaidia serikali kukomesha matukio hayo.

Akizungumza na watoto jana jijini Arusha, Mratibu wa Jinsia kutoka Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Linus Kahendaguza,​ alisema endapo vyombo vya habari vikiendelea kuandika na kuibua aina za ukatili wanaofanyiwa watoto na wanawake maeneo mbalimbali, itakuwa rahisi wahusika kuchukuliwa hatua.

Amesema serikali itaendelea kuzindua madawati hayo shuleni kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo, ikiwemo taasisi zisizo za kiserikali, ili kudhibiti ukatili wanaofanyiwa watoto nyumbani na shuleni.

“Vitendo vya ukatili vinavyotolewa taarifa ni asilimia 12​ pekee, hivyo wanahabari wana wajibu wa kuendelea kuandika na kuibua changamoto zinazowakabili wanawake na watoto pamoja na makundi maalum, ili kutokomeza madhila wanayofanyiwa,” amesema.

Kwa upande wake Wilbert Muchunguzi, ambaye ni mtaalam wa haki za watoto kutoka shirika la Save the Children, amesema shirika hilo litaendelea kutoa elimu mbalimbali kwa watoto, ili wajue haki zao na wapi pa kuzipata, ili kudhibiti ukatili hasa shuleni, nyumbani, ikiwemo kupinga unyanyasaji wa kimwili.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...