KAMA UTANI! SIMBA WAMEANZA ‘KUPINDUA MEZA’ KWA YANGA

Date:

Share post:

AMA hakika, hilo ndilo swali unaloweza kujiuliza kuelekea ‘Kariakoo Derby’ ya Jumapili ya wiki hii, Mei 3, 2026, itakayochezwa katika Uwanja wa Jenerali Isamuhyo, Mbweni jijini Dar es Salaam.

Katika ‘derby’ mbili za hivi karibuni, ni kama Wekundu wa Msimbazi wamekataa unyonge mbele ya vigogo wenzao hao wa soka la Tanzania.

Mechi mbili ambazo Simba wamegoma kufungwa ni hii ya hivi karibuni (Aprili 29, 2026) iliyochezwa Visiwani Zanzibar. Waliifunga Yanga bao 1-0 na kutwaa ubingwa wa Kombe la Muungano.

Mchezo mwingine wa derby ni ule wa Machi Mosi, 2026, ambapo kikosi cha Wekundu wa Msimbazi kilipata suluhu (0-0) mbele ya wapinzani wake hao.

Kabla ya mechi hizo za hivi karibuni, Simba ilikuwa imepoteza mara nne mfululizo mbele ya Yanga (1-0, 2-0, 1-0 na 1-0).

Je, katika mchezo wa wikiendi hii Simba itaendelea kujinasua au itarudi kwenye utumwa wake mbele ya wakongwe wenzao?

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

NAMIBIA YA MALIZA DENI LA IMF

Rais wa Namibia, Netumbo Nandi-Ndaitwah, ameiongoza nchi yake kufikia hatua muhimu ya kiuchumi baada ya kukamilisha malipo yote...

SERIKALI KUONGEZA UWEKEZAJI KWA WAKUNGA KUIMARISHA AFYA YA MAMA NA MTOTO NCHINI

Serikali kupitia Wizara ya Afya imejipanga kuendelea kuongeza uwekezaji katika mafunzo, ajira, motisha na mazingira ya kazi kwa...

POLISI KUENDELEA KUDHIBITI WAZUSHI MITANDAONI, LIKIIMARISHA ULINZI KUELEKEA DERBY YA SIMBA NA YANGA

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limetoa taarifa ya matukio mbalimbali ya kiusalama na kisheria,...

DKT. SAMIA AFANYA UTEUZI, UTENGUZI NA UHAMISHO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi na uhamisho wa baadhi...