DKT. SAMIA AFANYA UTEUZI, UTENGUZI NA UHAMISHO

Date:

Share post:

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi na uhamisho wa baadhi ya viongozi wa serikali katika wizara mbalimbali.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Mei 2, 2026 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka, Mhe. Dkt. Evaline Wilbard Munisi (Mb.) ameteuliwa kuwa Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu inayoshughulikia Kazi, Ajira na Mahusiano. Anachukua nafasi ya Mhe. Rahma Riyadh Kisau (Mb.) ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Katika mabadiliko hayo, Bw. Eliakim Chacha Maswi amehamishwa kutoka Wizara ya Katiba na Sheria na kwenda kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum.

Aidha, Dkt. John Antony Jingu amehamishwa kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwenda kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bw. Bakari S. Machumu.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

NAMIBIA YA MALIZA DENI LA IMF

Rais wa Namibia, Netumbo Nandi-Ndaitwah, ameiongoza nchi yake kufikia hatua muhimu ya kiuchumi baada ya kukamilisha malipo yote...

SERIKALI KUONGEZA UWEKEZAJI KWA WAKUNGA KUIMARISHA AFYA YA MAMA NA MTOTO NCHINI

Serikali kupitia Wizara ya Afya imejipanga kuendelea kuongeza uwekezaji katika mafunzo, ajira, motisha na mazingira ya kazi kwa...

POLISI KUENDELEA KUDHIBITI WAZUSHI MITANDAONI, LIKIIMARISHA ULINZI KUELEKEA DERBY YA SIMBA NA YANGA

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limetoa taarifa ya matukio mbalimbali ya kiusalama na kisheria,...

NYUMA YA PAZIA ‘KITANZI’ CHA MAREKANI KWA JOSEPH KABILA

WASHINGTON DC, MarekaniSERIKALI ya Marekani imetangaza vikwazo kwa Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC),...