POLISI KUENDELEA KUDHIBITI WAZUSHI MITANDAONI, LIKIIMARISHA ULINZI KUELEKEA DERBY YA SIMBA NA YANGA

Date:

Share post:

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limetoa taarifa ya matukio mbalimbali ya kiusalama na kisheria, ikiwemo hukumu ya kesi ya mauaji, kukamatwa kwa watuhumiwa wa taarifa za uongo mitandaoni pamoja na maandalizi ya ulinzi kuelekea mchezo mkubwa wa ligi kuu.

Katika tukio la kwanza, Polisi imeeleza kuwa Aprili 30, 2026, Mahakama ya Hakimu Mkazi Dar es Salaam (Masijala Ndogo) ilimhukumu kunyongwa hadi kufa Abdalah Mussa maarufu kama Mr. Blue, baada ya kupatikana na hatia ya kumuua kwa makusudi aliyekuwa mpenzi wake, Ezenia Kamana.

Tukio hilo lilitokea Agosti 19, 2024 katika eneo la Chang’ombe Maduka Mawili, Wilaya ya Temeke, ambapo mwili wa marehemu ulipatikana ukiwa umekatwakatwa na kutupwa katika maeneo ya Ununio, Kunduchi na Tegeta, wilayani Kinondoni.

Sambamba na hilo, Jeshi la Polisi limewakamata watu wanaodaiwa kuhusika na kusambaza taarifa za uongo mitandaoni, akiwemo Mocrine Julius maarufu kama mazidi mkazi wa Salasala, Kinondoni. Watuhumiwa hao wanashikiliwa kwa tuhuma za kueneza taarifa zilizolenga kuleta taharuki katika jamii.

Katika hatua nyingine, Polisi imetangaza kuimarisha ulinzi kuelekea mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Simba SC na Yanga SC utakaochezwa Mei 3, 2026 kuanzia saa 12:00 jioni katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo. Jeshi hilo limewataka mashabiki na wadau wa soka kuzingatia amani, nidhamu na kuepuka vitendo vyovyote vinavyoweza kuvuruga utaratibu wa mchezo huo.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

NAMIBIA YA MALIZA DENI LA IMF

Rais wa Namibia, Netumbo Nandi-Ndaitwah, ameiongoza nchi yake kufikia hatua muhimu ya kiuchumi baada ya kukamilisha malipo yote...

SERIKALI KUONGEZA UWEKEZAJI KWA WAKUNGA KUIMARISHA AFYA YA MAMA NA MTOTO NCHINI

Serikali kupitia Wizara ya Afya imejipanga kuendelea kuongeza uwekezaji katika mafunzo, ajira, motisha na mazingira ya kazi kwa...

DKT. SAMIA AFANYA UTEUZI, UTENGUZI NA UHAMISHO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi na uhamisho wa baadhi...

NYUMA YA PAZIA ‘KITANZI’ CHA MAREKANI KWA JOSEPH KABILA

WASHINGTON DC, MarekaniSERIKALI ya Marekani imetangaza vikwazo kwa Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC),...