RC MAKALLA AHIMIZA UWASILISHWAJI WA MICHANGO YA WAFANYAKAZI KWA WAKATI JIJINI ARUSHA

Date:

Share post:

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Amos Gabriel Makalla, Mei Mosi 2026 amewataka waajiri kuhakikisha wanawasilisha kwa wakati michango ya wafanyakazi katika mifuko ya hifadhi ya jamii kwa mujibu wa sheria za nchi.

Akizungumza kwenye kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid jijini Arusha, Mhe. Makalla pia alisisitiza umuhimu wa wafanyakazi kuwajibika kazini ili wawe na msingi imara wa kudai haki zao.

Aidha, amehimiza uadilifu na ushirikiano mzuri kati ya waajiri na wafanyakazi, pamoja na kubainisha kuwa hali hiyo ni muhimu katika kufikia malengo ya maendeleo ya taasisi na taifa kwa ujumla huku akikemea vitendo vya uharibifu wa miundombinu ya huduma za kijamii na kuagiza hatua kali zichukuliwe dhidi ya watakaobainika kufanya vitendo hivyo.

Katika hatua nyingine, Mhe. Makalla amewataka wananchi wa Arusha kujipanga kunufaika na ujio wa mkutano wa kimataifa wa Bunge la Dunia (IPU), unaotarajiwa kufanyika Oktoba 3 hadi 10, 2026 katika Arusha International Conference Centre (AICC).

Amesema zaidi ya wajumbe 3,000 wanatarajiwa kushiriki mkutano huo, hivyo ni fursa kubwa kwa wakazi wa Arusha, hususan katika sekta za biashara, usafiri, utalii na huduma za malazi.
“Aliyepo sokoni atafaidika kwa sababu hoteli zitanunua bidhaa kwa ajili ya vyakula, mwenye usafiri atafaidika na mwenye hoteli naye atafaidika. Huu ni mnyororo wa thamani utakaomgusa kila mtu,” amesema Makalla.

Mbali na hayo Makalla ameongeza kuwa wageni wengi watakaohudhuria watakuja pia na familia zao na huenda wakatenga muda wa kutembelea vivutio vya utalii, hivyo kutoa wito kwa wadau wa sekta hiyo na wafanyakazi kwa ujumla kutoa huduma bora ili kuendelea kuitangaza Tanzania kama nchi salama na yenye kuvutia kwa uwekezaji na utalii.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

NAMIBIA YA MALIZA DENI LA IMF

Rais wa Namibia, Netumbo Nandi-Ndaitwah, ameiongoza nchi yake kufikia hatua muhimu ya kiuchumi baada ya kukamilisha malipo yote...

SERIKALI KUONGEZA UWEKEZAJI KWA WAKUNGA KUIMARISHA AFYA YA MAMA NA MTOTO NCHINI

Serikali kupitia Wizara ya Afya imejipanga kuendelea kuongeza uwekezaji katika mafunzo, ajira, motisha na mazingira ya kazi kwa...

POLISI KUENDELEA KUDHIBITI WAZUSHI MITANDAONI, LIKIIMARISHA ULINZI KUELEKEA DERBY YA SIMBA NA YANGA

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limetoa taarifa ya matukio mbalimbali ya kiusalama na kisheria,...

DKT. SAMIA AFANYA UTEUZI, UTENGUZI NA UHAMISHO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi na uhamisho wa baadhi...