Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel Gideon Sa’ar amesema nchi yake haina nia ya kutwaa maeneo ya Lebanon, wakati vikosi vya Israel vikiendelea na operesheni kusini mwa nchi hiyo dhidi ya kundi la Hezbollah linaloungwa mkono na Iran, licha ya kuwepo kwa makubaliano ya kusitisha mapigano.
“Israel haina matarajio ya kujitanua kimamlaka au kutwaa maeneo ya Lebanon,” Sa’ar alisema katika mkutano wa pamoja na mwenzake wa Serbia, Marko Đurić.
“Uwepo wetu katika maeneo ya mpakani kaskazini una lengo moja tu: kuwalinda raia wetu.”






