PSG YAILAZA BAYERN MUNICH BAO 5-4 FAINALI YA KWANZA LIGI YA MABINGWA ULAYA

Date:

Share post:

Klabu ya Paris Saint‑Germain ya Ufaransa imeipiga Bayern Munich ya Ujerumani 5-4 katika raundi ya kwanza ya mchezo wao wa Nusu Fainali, Ligi ya Mabingwa Ulaya. Hata hivyo miamba hao wa Ufaransa bado wana kibarua kigumu katika raundi ya pili ya mchezo wao ujao.

Kocha wa Paris Saint‑Germain Luis Enrique amesema timu yake italazimika kucheza kwa umakini mkubwa na kufunga mabao zaidi ugenini dhidi ya Bayern Munich wiki ijayo ili kuhakikisha inafuzu fainali nyingine ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Ameeleza kuwa mazingira ya ugenini Allianz Arena yanahitaji kiwango cha juu cha umakini na ubunifu wa kushambulia.

Mchezo huo wa kwanza umeingia kwenye historia kama nusu fainali yenye mabao mengi zaidi katika enzi ya sasa ya Ligi ya Mabingwa, ukionyesha ubora wa safu za ushambuliaji za timu zote mbili pamoja na changamoto katika safu zao za ulinzi.

Mashabiki na wachambuzi wa soka wameutaja mchezo huo kuwa moja ya mechi za nusu fainali zenye ushindani mkubwa na kusisimia kuwahi kutokea.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

SERIKALI YAIMARISHA USAMBAZAJI WA CHANJO IKIZINDUA BOTI 7 ZA BILION1.1

Serikali imeendelea kuimarisha huduma za chanjo nchini kupitia uzinduzi wa boti saba zenye thamani ya shilingi Bilioni 1.1...

VYOMBO VYA HABARI NCHINI VYA TAJWA KUWA NGUZO YA KULINDA MAADILI YA MTANZANIA

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amesema Serikali inavitegemea kwa kiasi kikubwa vyombo vya habari...

HANDENI KUIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA KUPITIA UGAWAJI WA VYANDARUA BURE

Katika kuendeleza jitihada za kupambana na ugonjwa wa malaria nchini, Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kwa kushirikiana na...

UZALISHAJI NA UINGIZAJI WA MIFUKO YA PLASTIKI WAPUNGUA KWA ASILIMIA 95%

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Reuben Kwagilwa bungeni jijini...