CUBA YALAANI VIKWAZO VIPYA VYA MAREKANI

Date:

Share post:

HAVANA, Cuba
WAZIRI wa Mambo ya Nje wa Cuba, Bruno Rodriguez, ameviita kuwa ni ukatili vikwazo vipya walivyowekewa na Marekani.

Jana Mei Mosi, 2026, Rais Donald Trump alisaini agizo la vikwazo vipya kwa viongozi wa sekta za nishati, ulinzi, fedha na ulinzi nchini Cuba.

Pia, vikwazo hivyo vimekumba baadhi ya viongozi waliotajwa na Marekani kujihusisha na vitendo vya rushwa na ukikwaji wa haki za binadamu.

Maagizo hayo yanakuja baada ya maandamano ya wafanyakazi nchini Cuba kufika nje ya ofisi za Ubalozi wa Marekani.

Hoja ya maandamano hayo ni kukosoa hatua ya Marekani kuzuia nishati ya mafuta kuingia Cuba, hali inayoathiri uchumi wa Taifa hilo na kupanda kwa gharama za maisha.

Kwa upande mwingine, Rais Trump amenukuliwa mara kadhaa akisema nia yake ni kuiondosha madarakani Serikali ya kijamaa inayokiongoza Kisiwa hicho.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

NAMIBIA YA MALIZA DENI LA IMF

Rais wa Namibia, Netumbo Nandi-Ndaitwah, ameiongoza nchi yake kufikia hatua muhimu ya kiuchumi baada ya kukamilisha malipo yote...

SERIKALI KUONGEZA UWEKEZAJI KWA WAKUNGA KUIMARISHA AFYA YA MAMA NA MTOTO NCHINI

Serikali kupitia Wizara ya Afya imejipanga kuendelea kuongeza uwekezaji katika mafunzo, ajira, motisha na mazingira ya kazi kwa...

POLISI KUENDELEA KUDHIBITI WAZUSHI MITANDAONI, LIKIIMARISHA ULINZI KUELEKEA DERBY YA SIMBA NA YANGA

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limetoa taarifa ya matukio mbalimbali ya kiusalama na kisheria,...

DKT. SAMIA AFANYA UTEUZI, UTENGUZI NA UHAMISHO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi na uhamisho wa baadhi...