SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR KUENDELEZA USHIRIKIANO NA IRELAND

Date:

Share post:

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Zanzibar itaendelea kuimarisha ushirikiano wa muda mrefu na Ireland, hususan katika sekta za uwekezaji, biashara, uchumi wa buluu, utalii na ustawi wa jamii.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 30 Aprili 2026, alipokutana na Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Balozi Nicola Brennan, Ikulu Zanzibar, ambapo pia ameishukuru Ireland kwa mchango wake katika sekta za afya, elimu na sheria.

Aidha, amewakaribisha wawekezaji kutoka Ireland kuja kuwekeza Zanzibar katika sekta mbalimbali za maendeleo, huku akisisitiza umuhimu wa kuendeleza na kuhifadhi Mji Mkongwe kama urithi wa kihistoria na kivutio cha utalii.

Kwa upande wake, Balozi Brennan amepongeza maendeleo ya Zanzibar na kuahidi kuendeleza ushirikiano pamoja na kuongeza fursa za mafunzo, hususan katika sekta ya sheria.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

RAIS DKT. MWINYI APOKEA RIPOTI YA CAG ZANZIBAR YA MWAKA 2024/2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameipokea Ripoti ya Mdhibiti...

KAMBI YA WAKIMBIZI NDUTA KUFUNGWA KUFUATIA UREJESHWAJI WA HIARI WA WAKIMBIZI BURUNDI

Kambi ya Wakimbizi ya Nduta iliyopo Wilaya ya Kibondo, Mkoa wa Kigoma inatarajiwa kufungwa rasmi Leo Aprili 30,...

INTANETI YA KASI YAFIKIA ASILIMIA 94 MAENEO YA MAKAZI WATUMIAJI WAKIFIKA ASILIMIA 85.3

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Angellah Kairuki, amesema huduma ya intaneti ya kasi imefikia asilimia 94...

SERIKALI KUSHIRIKIANA NA WADAU KUTOA ELIMU YA UPANDAJI MITI KWA BIASHARA YA KABONI

Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeendelea kufanya jitihada mbalimbali ili kuhakikisha...