WAZIRI MKUU AWASILI ARUSHA KWA ZIARA YAKE YA KIKAZI

Date:

Share post:

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amewasili mkoani Arusha kwa ziara ya kikazi ya siku mbili, akilenga kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo.

Dkt. Nchemba aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Arusha leo Aprili 17, 2026, ambapo alipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Nurdin Babu, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla.

Katika siku ya kwanza ya ziara yake, Waziri Mkuu anatarajiwa kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu wa AFCON 2027, pamoja na miradi ya miundombinu ikiwemo ujenzi wa Barabara ya Mzunguko (Ring Road) kipande cha Mbauda – Oljoro hadi eneo la Fun Retreat, jijini Arusha.

Aidha, katika siku ya pili ya ziara hiyo, Aprili 18, 2026, Dkt. Nchemba atakuwa mgeni rasmi katika mkutano wa Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati (SMEs), utakaofanyika katika Hoteli ya Four Point, jijini Arusha.

Ziara hiyo inalenga kuhimiza utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na kukuza shughuli za kiuchumi katika mkoa wa Arusha na maeneo ya jirani.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

MAREKANI, CUBA: MZOZO MWINGINE UNAOSUBIRI KUITIKISA DUNIA

HAVANA, CubaRAIS wa Cuba, Miguel Diaz-Canel, hajaonesha unyonge, licha ya Taifa lake kuendelea kupewa presha kubwa na Rais...

LINDI YAIMARISHA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA WASH KUBORESHA AFYA ZA WANANCHI

Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zuwena Omary, amesema mkoa huo unaendelea kunufaika na utekelezaji wa afua...

BARAZA LA MADIWANI MTAMA LAKUTANA, LAPONGEZA MAFANIKIO YA MIRADI YA MAENDELEO

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama limefanya kikao chake cha robo ya tatu kwa mwaka...

VIONGOZI LONGIDO WATAKIWA KUHARAKISHA UANZISHAJI WA JUHIZINA

Viongozi wa vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Longido wametakiwa kuongeza kasi ya utekelezaji wa mchakato wa kuanzisha...