KLOPP, POCHETTINO NANI KUPEWA KAZI MADRID?

Date:

Share post:

LONDON, Uingereza
MABOSI wa Real Madrid wanatembea na majina ya makocha wawili, Jurgen Klopp na Mauricio Pochettino, na huenda mmoja wao akaajiriwa kuinoa timu hiyo.

Madrid kwa sasa iko chini ya kocha wa muda, Alvaro Arbeloa, ambaye atamaliza majukumu yake mwishoni mwa msimu huu.

Gazeti la Daily Mail limeripoti kuwa Rais wa klabu hiyo, Florentino Perez, anavutiwa na makocha wote, Klopp na Pochettino.

Madrid imeondoshwa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na tayari imeachwa pointi tisa na Barcelona iliyojichimbia kileleni mwa msimamo wa La Liga.

Klopp bado yuko nje ya kazi ya ukocha, wakati Pochettino ni kocha wa timu ya Taifa ya Marekani inayojiandaa na fainali zijazo za Kombe la Dunia.

Imeandaliwa na Hassan Mwasha

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

VIONGOZI LONGIDO WATAKIWA KUHARAKISHA UANZISHAJI WA JUHIZINA

Viongozi wa vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Longido wametakiwa kuongeza kasi ya utekelezaji wa mchakato wa kuanzisha...

LIGI YA EUROPA KUMEKUCHA NUSU FAINALI

LONDON, UingerezaMECHI za marudiano hatua ya robo fainali ya msimu huu wa Ligi ya Europa zilimalizika usiku wa...

MAZUNGUMZO YA ISRAEL, LEBANON KUITULIZA HEZBOLLAH?

BEIRUT, LebanonRAIS wa Marekani, Donald Trump, ameutangazia ulimwengu kuwa viongozi wa Israel na Lebanon wameifikia makubaliano ya kusitisha...

MTANDA AKUTANA NA UONGOZI NA JMAT, KUWAASA USHIRIKIANO NA AMANI

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano...