KANE AWEKA REKODI AKIIPELEKA BAYERN NUSU FAINALI ULAYA

Date:

Share post:

MUNICH, Ujerumani
STRAIKA wa Bayern Munich, Harry Kane, amekuwa mchezaji wa kwanza raia wa England kufikisha mabao 12 katika msimu mmoja wa michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Kane aliweka rekodi hiyo jana Aprili 15, 2026 alipofunga moja wakati Bayern ikiitandika Real Madrid mabao 4-3 na kutinga nusu fainali ya mashindano hayo.

Mchezo huo ulikuwa ni wa robo fainali ya pili baada ya ule wa kwanza uliochezwa Hispania kumalizika kwa Bayern kushinda mabao 2-1.

Kwa msimu huu pekee, Kane ameshaingia wavuni mara 50 katika mechi 42 za mashindano mbalimbali alizocheza akiwa na Bayern.

Msimu wa 2024-25, nyota huyo wa zamani wa Tottenham aliweka rekodi ya kuwa Muingereza wa kwanza kufunga mabao 11 katika msimu mmoja wa Ligi ya Mabingwa.

Imeandaliwa na Hassan Mwasha

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

UCHUMI WA CHINA WAZIDI KUIMARIKA

BEIJING, China LICHA ya vita vya Marekani na Iran kuonekana kuitikisa dunia, China imeendelea kupiga hatua kubwa katika eneo...

SIKU 100 ZA RAIS MPYA WA VENEZUELA: MABADILIKO NA MASWALI MAPYA

CARACAS, Venezuela BAADA ya vikosi vya Marekani kumng’oa madarakani aliyekuwa Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro kwenye oparesheni ya Januari...

MAELFU YA FAMILIA SUDAN BADO WAKIMBIA VITA, HALI YA MAISHA YAZIDI KUWA MBAYA

MAELFU ya familia nchini Sudan bado wanalazimika kuyakimbia makazi yao, miji na hata mipaka ya nchi kufuatia vita...

ISRAEL YAENDELEA NA OPERESHEN DHIDI YA HEZBOLLAH NCHINI LEBANON

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema Jeshi la nchi yake linaendelea na operesheni dhidi ya wanamgambo wanaoungwa...