PSG YAMWACHIA ‘MSALA’ KOCHA WA LIVERPOOL

Date:

Share post:


MERSEYSIDE, Uingereza
KICHAPO cha mabao 2-0 kutoka kwa PSG kimeongeza presha kwa kocha wa Liverpool, Arne Slot, ikielezwa kuwa huenda Mholanzi huyo akafungashiwa virago hivi karibuni.

Wakiwa nyumbani Anfield, Liverpool walikubali kipigo hicho kilichowasukuma nje ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, waliishia hatua ya robo fainali.

Katika mechi ya kwanza iliyocheza jijini Paris wiki moja iliyopita, PSG walipata ushindi kama huo, hivyo sasa wametinga hatua ya nusu fainali.

Kwa matokeo hayo, Liverpool imefikisha mechi 17 ilizopoteza msimu huu, takwimu zinazoongeza presha kwa Slot kutimuliwa.

Kocha anayepewa nafasi kubwa ya kuchukua mikoba yake pale Anfield ni kiungo wa zamani wa klabu za Liverpool, Bayern Munich na Real Madrid, Xabi Alonso.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...