YAMAL AVUNJA REKODI MBILI USIKU WA ULAYA

Date:

Share post:

MADRID, Hispania

LICHA ya Barcelona kung’olewa Ligi ya Mabingwa Ulaya, kinda wake wa safu ya ushambuliaji, Lamine Yamal, ameitumia mechi yao dhidi ya Atletico Madrid kuweka rekodi mbili.

Barcelona walikwenda ugenini wakiwa na kumbukumbu mbaya ya kufungwa mabao 2-0 katika robo fainali ya kwanza. Walishinda mabao 2-1 jana Aprili 14, 2026 lakini wametolewa kwa matokeo ya jumla (3-2).

Wakiwa ugenini jana, Yamal aliitanguliza Barcelona katika dakika ya nne tu ya mchezo, akitumia ‘asisti’ ya Ferran Torres.

Hivyo, Mhispania huyo amekuwa mchezaji mwenye umri mdogo zaidi (miaka 18 na siku 275) kufikisha mabao 20 kwenye michuano hiyo ya Ligi ya Mabingwa.

Wakati huo huo, Yamal amekuwa mchezaji mwenye umri mdogo zaidi kupachika mabao 10 ndani ya msimu mmoja wa mashindano hayo ya Shirikisho la Soka la Ulaya (UEFA).

Awali, rekodi hiyo ilikuwa ikishikiliwa na Erling Haaland aliyefanya hivyo akiwa na miaka 19 na siku 212, wakati huo akiitumikia Red Bull Salzburg ya Austria.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...