BEAUMELLE AKIRI UGUMU WA SUNDOWNS, AWAHIMIZA WACHEZAJI WAKE KUPAMBANA

Date:

Share post:

Kocha mkuu wa klabu ya Espérance Sportive de Tunis, Patrice Beaumelle, amekiri kuwa kikosi chake kinakabiliwa na changamoto kubwa kuelekea mchezo wa marudiano wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) dhidi ya Mamelodi Sundowns.

Beaumelle ametoa kauli hiyo kufuatia kupoteza mchezo wa kwanza uliopigwa nyumbani kwa bao 1-0, Jumapili, Aprili 12, 2026. Amesema matokeo hayo yanaakisi tofauti ya kiwango kati ya timu hizo mbili, akieleza kuwa Sundowns ni moja ya timu imara zaidi barani Afrika kwa sasa.

Akizungumza baada ya mchezo huo, Beaumelle alieleza kuwa kucheza dhidi ya timu yenye wachezaji wengi wenye uzoefu wa michuano ya kimataifa, ikiwemo waliocheza Kombe la Dunia la Klabu, ni mtihani mkubwa kwa klabu yoyote Afrika.

“Ni kweli kuna tofauti ya kiwango kwa kiasi fulani, lakini licha ya hilo, tulionyesha ushindani mkubwa dhidi ya timu yenye uzoefu mkubwa na yenye ubora wa hali ya juu,” alisema Beaumelle.

Kocha huyo raia wa Ufaransa aliwapongeza wachezaji wake kwa kupambana kwa juhudi katika mchezo huo, huku akisisitiza kuwa bado wana nafasi ya kupindua matokeo katika mchezo wa marudiano utakaochezwa Afrika Kusini Aprili 18, 2026.
Amesema kikosi chake kimejipanga kuhakikisha kinapata matokeo mazuri ugenini ili kufuzu hatua ya fainali ya mashindano hayo makubwa barani Afrika.

Iwapo Espérance itafanikiwa kusawazisha au kushinda kwa mabao ya kutosha, itatinga fainali ambapo itakutana na mshindi kati ya FAR Rabat na RS Berkane, zote kutoka Morocco.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...

ISHU YA RASHFORD BADO PASUA KICHWA

MANCHESTER, UingerezaKOCHA wa Manchester United, Michael Carrick, amesema bado haijafahamika kama Marcus Rashford atarudi klabuni hapo au atabaki...

BARCA YAPATA MRITHI WA LEWANDOWSKI

CATALUNYA, HispaniaKLABU ya Barcelona imeanza mipango ya kumsajili mshambuliaji wa kati wa Real Mallorca, Vedat Muriqi, ikiamini anatosha...

ARSENAL AKILI YOTE KWA MONGA

LONDON, UingerezaARSENAL ya Kaskazini mwa Jiji la London imeonesha nia ya kumsajili winga anayefanya vizuri Ligi Daraja la...