KINDA WA SOKA AUAWA KWA KUPIGWA RISASI

Date:

Share post:

ACCRA, Ghana

NYOTA wa kabumbu mwenye umri wa miaka 20 nchini Ghana ameuawa baada ya watu wasiojulikana kuvamia na kulishambulia kwa risasi basi la timu yake.

Winga huyo wa klabu maarufu ya Berekum Chelsea, Dominic Frimpong, amefariki baada ya kupigwa risasi ya kichwa katika tukio hilo.

Vyanzo vya habari vinaeleza kuwa basi la wachezaji hao lilikuwa njiani kuelekea kwa wapinzani wao wa mechi ijayo, FC Samartex.

Wakiwa Barabara ya Bibiani-Goaso, watu walioshika bunduki walivamia basi lao na kuanza kumimina risasi.

Baadhi ya wachezaji na viongozi walitorokea porini ili kunusuru maisha yao na wapo ambao hawajulikani walipo hadi sasa.

Frimpong amekuwa na kiwango bora msimu huu, akifunga mabao mawili katika mechi 11.

Imeandaliwa na Hassan Mwacha

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...