‎Klabu ya Manchester City imetangaza kuwa inafikiria kuchukua hatua za kisheria baada ya kuibuka kwa taarifa nchini Hispania zinazodai kuwa mshambuliaji wake nyota, Erling Haaland, anaweza kuhamia Real Madrid.

‎Hatua hiyo inakuja baada ya mwakilishi wa Haaland kukanusha vikali madai yaliyotolewa na mfanyabiashara wa Hispania Enrique Riquelme kuhusu uwezekano wa mchezaji huyo kujiunga na mabingwa hao wa La Liga.

‎Katika taarifa yake, Manchester City imeeleza kuwa taarifa hizo si za kweli na kusisitiza kuwa hakuna kifungu chochote katika mkataba wa Haaland kinachoruhusu uhamisho huo kwenda Real Madrid.

‎Aidha, klabu hiyo ya Ligi Kuu England imeonya kuwa inaweza kuchukua hatua za kisheria dhidi ya matumizi ya picha na jina la mchezaji wake katika taarifa zinazodaiwa kuwa za kupotosha umma.

‎Haaland bado anaendelea kuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Manchester City, huku klabu hiyo ikisisitiza kuwa mustakabali wake unaendelea kubaki ndani ya timu hiyo.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here