Ligi ya Mpira wa Kikapu ya Marekani (NBA) imeamsha kumbukumbu za mashabiki wake kuelekea mchezo wa kwanza wa Fainali za NBA kwa kuangazia baadhi ya viwanja vya kihistoria vilivyowahi kutumika katika hatua hiyo muhimu ya mashindano hayo.
Katika ujumbe wake, NBA imewahimiza mashabiki kutembea katika njia ya kumbukumbu kwa kuangalia viwanja mbalimbali vilivyoshuhudia historia kubwa ya Fainali za NBA kwa miaka tofauti.
Mashindano hayo yanarejea huku Kombe la Larry O’Brien, ambalo hutolewa kwa mabingwa wa NBA, likiwa kitovu cha ushindani.
Pia Fainali za mwaka huu zitawakutanisha New York Knicks na San Antonio Spurs, huku mchezo wa kwanza ukitarajiwa kuchezwa Leo usiku.
Mashabiki wa mpira wa kikapu duniani kote wanaisubiria fainali kwa hamu na kuwa na ushindani mkubwa katika kuwania taji la ubingwa wa NBA.







