Klabu ya Manchester United imefikia makubaliano ya kumsajili kiungo wa Atalanta, Ederson, katika dirisha la usajili la majira ya joto.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, United italipa euro milioni 45 pamoja na nyongeza mbalimbali ili kukamilisha uhamisho wa nyota huyo wa Brazil.
Aidha Ederson anatajwa kuwa niusajili wa kwanza chini ya kocha Michael Carrick katika maandalizi ya msimu mpya.
Mazungumzo kati ya pande hizo mbili yalidumu kwa wiki kadhaa kabla ya kufikia hatua ya makubaliano ya mwisho.
Mchezaji huyo anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka minne mara baada ya kukamilisha vipimo vya afya na taratibu nyingine za mwisho za uhamisho.
Usajili wa Ederson ni sehemu ya mkakati wa Manchester United wa kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao, huku mashabiki wakisubiri kuona mchango wake ndani ya dimba la Old Trafford.







