‎Timu ya taifa ya Mali, maarufu kama Les Aigles du Mali (Tai wa Mali), imeanza rasmi maandalizi yake kwa mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Iran utakaochezwa tarehe 4 Juni mjini Antalya, nchini uturuki.


‎Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ukurasa rasmi wa timu hiyo, wachezaji wa Mali walifanya kikao chao cha kwanza cha mazoezi alasiri huko Antalya.

‎Mazoezi hayo yalifanyika katika uwanja wa Gloria Sports Arena Complex, ambapo jumla ya wachezaji 20 walihudhuria na kushiriki kikamilifu.

‎Aidha chezo huo wa kirafiki dhidi ya Iran ni sehemu ya maandalizi ya timu ya Mali kwa mashindano na mechi zijazo za kimataifa.

‎Kwa upande wa Benchi la ufundi hilo linatarajia kutumia mechi hiyo kupima uwezo wa kikosi na kuimarisha mbinu mbalimbali kabla ya ratiba nyingine muhimu.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here