WAPIGA RAMLI CHONGANISHI SIMIYU WAONYA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI

Date:

Share post:

Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu limeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu madhara ya vitendo vya kishirikina vinavyohusisha upigaji wa ramli chonganishi pamoja na kujichukulia sheria mkononi.

Akizungumza Mei 15, 2026 katika kijiji cha Ng’hesha Wilaya ya Itilima, Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Simiyu Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Chacha Maro amesema baadhi ya waganga wa tiba asili wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya upigaji wa ramli chonganishi vinavyoweza kusababisha madhara makubwa ikiwemo mauaji, majeruhi na kusambaratika kwa familia.

ACP Maro amewataka wananchi pamoja na viongozi wa sungusungu kuacha kujichukulia sheria mkononi na badala yake kutoa taarifa kwenye vyombo vya dola pale wanapohisi kuwepo kwa viashiria vya uhalifu.

Aidha, amesisitiza kuwa Jeshi la Polisi halitasita kuwachukulia hatua kali za kisheria wote watakaobainika kuvunja sheria za nchi kwa namna yoyote ile.

Kwa upande wake, Afisa Tarafa ya Kanadi Lameck Lupiga amewahimiza wananchi kufuata taratibu za kisheria katika kutoa taarifa za uhalifu badala ya kutumia nguvu au kufanya maamuzi binafsi.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Ng’hesha, Bunga Nselema amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi, akisema hatua hiyo itasaidia kuimarisha amani na usalama katika kijiji hicho.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

MSONGO WA MAWAZO NI CHANZO CHA WANAFUNZI KUTUMIA MATUSI KATIKA MITIHANI

Serikali imesema imeanza kuchukua hatua mbalimbali kubaini chanzo cha tabia ya baadhi ya wanafunzi kuandika lugha zisizostahili kwenye...

FURSA 4 ZITAKAZILINUFAISHA TAIFA KUPITIA SEKTA YA UTALII

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji, amesema Tanzania inatarajia kunufaika kwa kiasi kikubwa kiuchumi kupitia utalii...

SERIKALI KUENDELEA KUNUNUA MELI MPYA NA KUKARABATI ZILIZOPO – PROF. MAKAME MBARAWA

WAZIRI wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, amesema Serikali kupitia TASHIKO imeendelea kusimamia ununuzi wa meli mpya, pamoja na...

SHUGHULI ZA UCHIMBAJI MADINI ZA SITISHWA KATIKA MITO YA MTISI NA IBANDA MKOANI KATAVI

Serikali imechukua hatua kali dhidi ya ukiukwaji wa sheria katika sekta ya madini baada ya Waziri wa Madini,...