BAYER, PSG, ARSENAL, ATLETICO NANI KUTINGA FAINALI?

Date:

Share post:

LONDON, Uingereza

ARSENAL watakuwa Emirates kuwakaribisha Atletico Madrid, mchezo wa nusu fainali ya pili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya utakaochezwa leo Mei 5, 2026.

Kesho, Bayern watakuwa nyumbani Allianz Arena kucheza na PSG, ikiwa ni nusu fainali nyingine ya marudiano baada ya ile iliyochezwa jijini Paris.

ARSENAL V ATLETICO

Arsenal ya kocha Mikel Arteta ilipata sare ya bao 1-1 ugenini nchini Hispania, hivyo safari hii Atletico Madrid wana kibarua kigumu cha kuhimili presha ya Emirates.

Hii itakuwa mara ya nne kwa Atletico kucheza katika ardhi ya Uingereza msimu huu, ambapo ilipoteza mechi zote tatu zilizopita.

Septemba, 2025, iliifuata Liverpool pale Anfield na kufungwa mabao 3-2. Mwezi uliofuata, ilitua Emirates na kubamizwa mabao 4-0. Baadaye, ilivaana na Tottenham jijini London na kufungwa mabao 3-2.

Msimu huu, Washika Bunduki wa London hawajafungwa katika mechi zote 15 za Ligi ya Mabingwa walizocheza, wakati Atletico imechezea vichapo vitano.

BAYERN V PSG

Mechi ya nusu fainali ya kwanza ilishuhudia mabao tisa yakifungwa jijini Paris wakati PSG ilipopata ushindi wa mabao 5-4. Safari hii, watakuwa mjini Munich, Ujerumani.

Timu hizo zitakutana zikiwa zimetoka kujeruhiwa katika Ligi za ndani. PSG ilimazimishwa sare ya mabao 2-2, wakati Bayern nao walipata sare ya 3-3 dhidi ya Heidenheim.

Bayern wanategemea safu yao ya ushambuliaji yenye Michael Olise, Harry Kane na Luis Diaz, ambayo imeshafunga mabao zaidi ya 100 msimu huu.

Mabingwa watetezi, PSG, wataikosa huduma ya Achraf Hakimi lakini pengo lake katika eneo la beki wa kulia, Warren Zaire-Emery, ambaye atakuwa na kibarua cha kumdhibiti Diaz.

Tangu ilipobadilishwa jina kutoka Kombe la Ulaya na kuitwa Ligi ya Mabingwa, Madrid ndiyo timu pekee iliyowahi kuwa mabingwa mara mbili mfululizo.

Hivyo, matajiri wa Ligue 1, PSG, wanaisaka rekodi hiyo baada ya kubeba ‘ndoo’ ya mashindano hayo ya Ligi ya Mabingwa msimu uliopita, walipoifunga Inter Milan mabao 5-0 katika mchezo wa fainali.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

RUTO ASISITIZA USHIRIKIANO WA EAC NI UFUNGUO WA KUKUZA BIASHARA NA AJIRA KWA WANANCHI

Rais wa William Ruto amesema nchi za Afrika Mashariki zina fursa kubwa ya kuongeza biashara ya ndani na...

WIZARA YA MAJI KUIMARISHA TEKNOLOJIA KUDHIBITI UPOTEVU WA MAJI NCHINI

Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, amesema Wizara yake itaendelea kuimarisha udhibiti wa upotevu wa maji katika mifumo ya...

MAPITIO MAPYA YA SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA YAFANYIKA KUOANISHA NA DIRA YA MAENDELEO YA TAIFA 2050

Wizara ya Fedha imeanza mchakato wa kupitia upya Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura ya 410, kwa lengo...

WANANCHI ZAIDI YA MILIONI 15 KUNUFAIKA NA TEKNOLOJIA YA KAMERA ZA FUNDUS

Zaidi ya wananchi milioni 15 hadi 20 wanatarajiwa kunufaika na matumizi ya teknolojia ya Kamera za Fundus (Portable...