MOTSEPE: CAF ICHUNGUZWE TUHUMA ZA RUSHWA

Date:

Share post:

CAIRO, Misri

RAIS wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Patrice Motsepe, amesema yuko tayari kuruhusu Taasisi hiyo kuchunguzwa juu ya tuhuma za rushwa.

Motsepe ameyasema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa soka na Serikali nchini Senegal.

Kauli ya Motsepe imekuja baada ya Serikali ya Senegal kuomba ufanyike uchunguzi juu ya vitendo vya rushwa ndani ya Shirikisho hilo.

Ombi la Senegal lilikuja baada ya timu yao ya Taifa kuvuliwa ubingwa wa fainali za AFCON 2025, taji ambalo walikabidhiwa Morocco.

Akizungumza na viongozi wa Shirikisho la Soka la Senegal, pamoja na Rais wa nchi hiyo, Bassirou Diomaye Faye, Motsepe amesema: “Nakaribisha uchunguzi wa rushwa, iwe utafanywa na Serikali au taasisi binafsi.”

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...