{"id":422,"date":"2021-12-24T05:09:00","date_gmt":"2021-12-24T05:09:00","guid":{"rendered":"https:\/\/msangirstz8.wordpress.com\/2021\/12\/24\/tra-yatoa-msimamo-lugha-ya-kichina-kwenye-risiti-za-efd\/"},"modified":"2021-12-24T05:09:00","modified_gmt":"2021-12-24T05:09:00","slug":"tra-yatoa-msimamo-lugha-ya-kichina-kwenye-risiti-za-efd","status":"publish","type":"post","link":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/?p=422","title":{"rendered":"TRA YATOA MSIMAMO LUGHA YA KICHINA KWENYE RISITI ZA EFD"},"content":{"rendered":"<table align=\"center\" cellpadding=\"0\" cellspacing=\"0\" class=\"tr-caption-container\" style=\"margin-left:auto;margin-right:auto;\">\n<tbody>\n<tr>\n<td style=\"text-align:center;\"><a href=\"https:\/\/blogger.googleusercontent.com\/img\/a\/AVvXsEjMIdB5D6DkemZYrzrbnuP6FdFfpE6R04hPZsSa0ZZSTTl2wWBdRJTnKoLZSc3AGIsP6SECHnicyS94CpDkJy3p0ZDsnnTg-ovb3K312CfQULxo6dqwlBKKPTXdI-S4l-IVkS03rg4zZSiJy8pWL6iZ_oVtacmSn_RBj7MIta1c0cBnUkJ2jshm91OC9g=s497\" style=\"margin-left:auto;margin-right:auto;\" target=\"_blank\" rel=\"noopener\"><img loading=\"lazy\" decoding=\"async\" border=\"0\" height=\"382\" src=\"https:\/\/blogger.googleusercontent.com\/img\/a\/AVvXsEjMIdB5D6DkemZYrzrbnuP6FdFfpE6R04hPZsSa0ZZSTTl2wWBdRJTnKoLZSc3AGIsP6SECHnicyS94CpDkJy3p0ZDsnnTg-ovb3K312CfQULxo6dqwlBKKPTXdI-S4l-IVkS03rg4zZSiJy8pWL6iZ_oVtacmSn_RBj7MIta1c0cBnUkJ2jshm91OC9g=w640-h382\" width=\"640\" \/><\/a><\/td>\n<\/tr>\n<tr>\n<td class=\"tr-caption\" style=\"text-align:center;\">Richard Kayombo<\/td>\n<\/tr>\n<\/tbody>\n<\/table>\n<p>\u00a0<!--[if gte mso 9]&gt;   Normal  0          false  false  false    EN-US  X-NONE  X-NONE                                       MicrosoftInternetExplorer4                                     &lt;![endif]--><!--[if gte mso 9]&gt;                                                                                                                                                                                                                                                                                    &lt;![endif]--><!--[if gte mso 10]&gt; \/* Style Definitions *\/  table.MsoNormalTable \t{mso-style-name:\"Table Normal\"; \tmso-tstyle-rowband-size:0; \tmso-tstyle-colband-size:0; \tmso-style-noshow:yes; \tmso-style-priority:99; \tmso-style-qformat:yes; \tmso-style-parent:\"\"; \tmso-padding-alt:0in 5.4pt 0in 5.4pt; \tmso-para-margin-top:0in; \tmso-para-margin-right:0in; \tmso-para-margin-bottom:10.0pt; \tmso-para-margin-left:0in; \tline-height:115%; \tmso-pagination:widow-orphan; \tfont-size:11.0pt; \tfont-family:\"Calibri\",\"sans-serif\"; \tmso-ascii-font-family:Calibri; \tmso-ascii-theme-font:minor-latin; \tmso-fareast-font-family:\"Times New Roman\"; \tmso-fareast-theme-font:minor-fareast; \tmso-hansi-font-family:Calibri; \tmso-hansi-theme-font:minor-latin;} &lt;![endif]--> <\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span><\/span><span style=\"font-size:large;\"><span>RIPOTA PANORAMA<\/span> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>0711 46 49 84<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>\u00a0<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>MAMLAKA ya Mapato (TRA) imetoa msimamo wa lugha zinazopaswa kutumika kwenye risiti zinazotolewa na mashine zote za kielekitroniki hapa nchni.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Imesema risiti zote za kielekitroniki zinazotolewa kwa wateja zinatakiwa zitumie lugha rasmi ambazo ni Kiingereza na Kiswahili na si vinginevyo.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Msimamo huo wa TRA umetolewa jana na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA, Richard Kayombo alipokuwa akijibu maswali aliyoulizwa na Tanzania PANORAMA Blog kuhusu duka kubwa la kuuza mahitaji ya nyumbani (Supermarket) inayofahamika kwa jina la Tai Le China Supermarket, iliyopo Mikocheni, Wilaya ya Kinondoni, Mkoa wa Dar es Salaam kutoa risiti za kielekitroniki zenye maandishi ya kichina.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Tanzania PANORAMA ilimuiliza Kayombo kuwa TRA imeanzisha lini utaratibu wa kutoa risiti zinazosoma maandishi ya lugha za kigeni na lugha ngapi za kigeni zilizoidhinishwa kutumika.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Katika majibu yake mafupi aliyoyatoa jana jioni, Kayombo alisema; \u201cRisiti zote zinatakiwa zitumie lugha rasmi ambazo ni Kiingereza na Kiswahili na si vinginevyo.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>\u201cNingependa kujua jina la supermarket hii ili meneja wetu wa Kinondoni alifanyie kazi.\u201d<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Wakati Kayombo akiomba jina la supermarket hiyo ili aliwasilishe kwa meneja wa TRA Kinondoni, Afisa Afya wa Kata ya Mikocheni, Fredy Ernest, mapema jana aliiambia Tanzania PANORAMA kuwa tayari maafisa wa taasisi hiyo wapo kwenye supermarket hiyo na kwamba alikuwa ameitwa kwenda hapo.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Tanzania PANORAMA ilimweleza Kayombo kuwa linazo taarifa kuwa tayari maafisa wa TRA wamekwishafika eneo hilo na ilimuomba aeleze walichobaini; swali hilo Kayombo hakulijibu.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span><\/p>\n<table align=\"center\" cellpadding=\"0\" cellspacing=\"0\" class=\"tr-caption-container\" style=\"margin-left:auto;margin-right:auto;\">\n<tbody>\n<tr>\n<td style=\"text-align:center;\"><a href=\"https:\/\/blogger.googleusercontent.com\/img\/a\/AVvXsEg4GtEKquDyGTH3f1s2dIJvqZwYJWZOujIBXzy4vu2fD_y0YvbB4wwqN0diby_N3Sjj2kvbu9p6tT4YC__D2DVLhdD0fFCvuo7JSXJ0tzionrXeZBP7wjRq3c01A1_lcenRZWfcZK0bHc6oJmCzX11FeyBPpsMYHJYoNRpxKPIpmetaq9vkJmE9f0PBcg=s660\" style=\"margin-left:auto;margin-right:auto;\" target=\"_blank\" rel=\"noopener\"><img loading=\"lazy\" decoding=\"async\" border=\"0\" height=\"320\" src=\"https:\/\/blogger.googleusercontent.com\/img\/a\/AVvXsEg4GtEKquDyGTH3f1s2dIJvqZwYJWZOujIBXzy4vu2fD_y0YvbB4wwqN0diby_N3Sjj2kvbu9p6tT4YC__D2DVLhdD0fFCvuo7JSXJ0tzionrXeZBP7wjRq3c01A1_lcenRZWfcZK0bHc6oJmCzX11FeyBPpsMYHJYoNRpxKPIpmetaq9vkJmE9f0PBcg=w640-h320\" width=\"640\" \/><\/a><\/td>\n<\/tr>\n<tr>\n<td class=\"tr-caption\" style=\"text-align:center;\">Kamishna Mkuu wa TRA, Alphayo Kidata<\/td>\n<\/tr>\n<\/tbody>\n<\/table>\n<p>\u00a0<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Awali, Kamishna Mkuu wa TRA Alphayo Kidata ambaye aliulizwa pia kuhusu <span>\u00a0<\/span>suala hilo, aliitaka Tanzania PANORAMA kuwasiliana na Kayombo ili aweze kutoa majibu.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Mmoja wa wafanyakazi katika supermarket hiyo (jina linahifadhiwa) aliyezungumza na Tanzania PANORAMA alisema duka hilo lipo muda mrefu na utaratibu wake ni huo siku zote na maafisa wa serikali hufika kufanya ukaguzi na kuondoka hivyo anashangaa habari zao kuanza kuandikwa sasa.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>\u201cMnajisumbua tu nyinyi, hii supermarket ipo hapa zaidi ya miaka mitatu na huu ndiyo utaratibu wao. Maafisa wa TRA, TBS hao OSHA wote wanakuja hapa kukagua na wanawaacha sisi nyie kuanza hizi hekaheka mnahangaika tu.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>\u201cNi wajanja sana hawa, hivi kama wameweza kuwepo miaka mitatu nyie mtaweza leo? Tangu jana mpaka leo mnadhani watakuwa hawajabadilisha hizo mashine? Kwani kuweka hizo lebo inachukua muda gani? Kwani wao ni wajinga? Hili duka japo limejificha humu ndani lakini lina wateja wengi sana tena wakubwa.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>\u201cWenzenu huwa wanakuja wanaongea nao wanaondoka sasa nyie mmeng\u2019ang\u2019ania. Mnajihangaisha tu,\u201d alisema. <span>\u00a0<\/span><\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Juzi, Tanzania PANORAMA Blog liliigundua Supermarket hiyo ikiwa na kibao kinachoitambulisha kwa jina la Tai Le China Supermarket katika eneo la Migombani, Kata ya Mikocheni na inamilikiwa na raia wa China aliyejitambulisha kwa jina moja la Wang.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Katika uchunguzi wake ndani ya supermarket hiyo, Tanzania PANORAMA ilibaini bidhaa zake nyingi zimeandikwa kwa lugha ya kichina pekee na hazijawekewa bei yoyote kwa mnunuzi (price tag) kama ulivyo utaratibu wa kawaida.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Baadhi ya bidhaa hizo ni mayai yenye rangi ya kijani kutoka China na yale yanayozalishwa hapa nchini, maziwa, dawa mbalimbali za mswaki, vinywaji baridi, pombe za aina mbalimbali na vyakula vya aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na nyama.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Aidha, uchunguzi ulibaini risiti za kielekitroniki zinazotolewa na supermarket hiyo zinaandikwa kichina isipokuwa bei ya jumla ya bidhaa inayouzwa inaandikwa kwa Lugha ya Kiswahili.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Meneja wa Tai Le supermarket,<span>\u00a0 <\/span>aliyejitambulisha kwa jina moja la Khadija alisema duka hilo ni maalumu kwa ajili ya raia wa China pekee.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Khadija alisema bidhaa nyingi zinazouzwa hapo zinaagizwa kutoka China yakiwemo mayai yenye rangi ya kijani na taratibu zote za usajili na kufanya biashara zimefuatwa ikiwemo kupatiwa vibali kutoka serikalini.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>\u201cHili duka ni kwa ajili ya raia wa China tu, halitoi huduma kwa watanzania. Ukiona mtanzania kaja hapa basi huyo ni mfanyakazi wa ndani katika nyumba za mchina au mtanzania aliyeishi China miaka mingi. <\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>\u201cKama unasema ulikuwa na shida na bidhaa lakini hujaona bei yake kwanza jua umeingia katika duka ambalo wewe halikuhusu kwa sababu wewe siyo mchina lakini bei za humu haziandikwi kwa sababu wachina wenyewe wanajua bei zao ndiyo maana unaona wanalipa na wanaondoka bila shida.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>\u201cIla kwa faida yako, humu hatuweki bei ya bidhaa kwa sababu katika siku za karibuni bei zinabadilika mara kwa mara, hivyo tunaweza kuweka leo kesho ikatulazimu kubadilisha tena, inakuwa ni usumbufu. Kwa hiyo bidhaa zetu tunauza kwa bei ya siku hiyo na unazipata hapo kaunta unapokwenda kulipia,\u201d alisema Khadija.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Mmiliki wa Supermarket hiyo, yeye alisema duka lake lina msemaji ambaye ni Ofisi ya Mtendaji Kata ya Mikocheni.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span><\/p>\n<table align=\"center\" cellpadding=\"0\" cellspacing=\"0\" class=\"tr-caption-container\" style=\"margin-left:auto;margin-right:auto;\">\n<tbody>\n<tr>\n<td style=\"text-align:center;\"><a href=\"https:\/\/blogger.googleusercontent.com\/img\/a\/AVvXsEhv1P1cVfN4nGhJpCeJkfnDBHB6E8JfXQnEsHYOZJlgvYOgOQu3oCEPi11ZtLTloOV0FJnTg0QjJF2kMg2IzgdpYK_hApemv_PWhCbmQ61X8N2_IvEUjtkdVDuBgm1867aWrmxBQ7Oac9B6KSKxoJTE6q0ZeY1X_tRK0m50mCByrU66TGr-FhK9DIuHIQ=s1080\" style=\"margin-left:auto;margin-right:auto;\" target=\"_blank\" rel=\"noopener\"><img loading=\"lazy\" decoding=\"async\" border=\"0\" height=\"426\" src=\"https:\/\/blogger.googleusercontent.com\/img\/a\/AVvXsEhv1P1cVfN4nGhJpCeJkfnDBHB6E8JfXQnEsHYOZJlgvYOgOQu3oCEPi11ZtLTloOV0FJnTg0QjJF2kMg2IzgdpYK_hApemv_PWhCbmQ61X8N2_IvEUjtkdVDuBgm1867aWrmxBQ7Oac9B6KSKxoJTE6q0ZeY1X_tRK0m50mCByrU66TGr-FhK9DIuHIQ=w640-h426\" width=\"640\" \/><\/a><\/td>\n<\/tr>\n<tr>\n<td class=\"tr-caption\" style=\"text-align:center;\">Eneo ilipo supermarket ya TaiLe<\/td>\n<\/tr>\n<\/tbody>\n<\/table>\n<p>\u00a0<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>\u201cMimi siruhusiwi kusema lolote, yupo msemaji wa duka hili. Yeye atakujibu au atakupa kibali uje nacho hapa ndiyo mimi nizungumze. Nenda Ofisi ya Mtendaji wa Kata, hao ndio watawapa majibu, mimi siwezi kuzungumza na ninyi. Serikali Kata ndiyo wanaweza kuwapa kibali cha kufika kwangu, kuingia hapa na kuniuliza. Ni hapo mtaa wa nyuma nendeni mkaongea na hao,\u201d alisema Wang.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Tanzania PANORAMA ambayo ilifika Ofisi ya Mtendaji Kata ya Mikocheni kufuatilia suala hilo na kuelekezwa kuzungumza na Afisa Afya wa Kata ya Mikocheni, Ernest ambaye alikiri kulifahamu duka hilo na kusema kuwa bidhaa zote zinazouzwa hapo ni halali na zina vibali vyote vya mamlaka za serikali vinavyohitajika.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Alisema duka hilo ni maalumu kwa ajili ya raia wa China peke yao na kwamba haliwahusu watanzania.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>\u201cKwanza nashangaa mmefikaje huko na kuanza kufanya ukaguzi, nani amewaruhusu kwenda huko? Sisi ndio tuna mamlaka ya kuwaruhusu kuuliza maswali sio kufika na kuanza kuhoji, hiyo<span>\u00a0 <\/span>siyo kazi yenu, lazima mpate kibali kutoka hapa.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>\u201cTambua hiyo supermarket ni kwa ajili ya wachina tu, sio kwa ajili ya watanzania na ukiona mtu mweusi hapo basi huyo katumwa na mchina au aliwahi kuishi huko sasa amekwenda kununua bidhaa anazozijua. Watanzania hapo sio kwao,\u201d alisema.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Alisema Mamlaka ya Udhibiti wa Bidhaa (TBS) ndiyo iliyotoa kwa Tai Le kibali cha kuingiza bidhaa zao nchini na kuuza zikiwa zimeandikwa kwa lugha ya kichina bila kulazimiki kuandika bei na kwamba maafisa wa taasisi za serikali hufanya ukaguzi kila mara.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Akizungumzia bei kutowekwa kwenye bidhaa alisema wanaopaswa kujibu ni TRA. <\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>\u201cLakini labda hilo la kuweka bei kwenye bidhaa wanazouza kama inavyohitajika, najua lipo kisheria, sasa hili niseme kwamba siwezi kuliongelea, nenda kawaulize Mamlaka ya Mapato ambao wamewapa kibali na huwa wanakuja kukagua, wanajua kwanini mashine zao za kielektoniki zinaandika kichina, wao ndiyo watakupa ufafanuzi.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>Aidha, Ernest alionya kuwa katika eneo la Kata ya Mikocheni waandishi wa habari hawaruhusiwa kufika kufanya kazi bila kupata kibali kutoka kwenye Ofisi ya Kata na kwamba mwandishi anayekiuka hilo anakiuka taratibu zilizowekwa na Serikali ya Wilaya ya Kinondoni.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>\u201cWako waandishi waliongia katika eneo la kata yangu na kuanza kuhoji watu bila kupitia ofisini kwangu. Ofisi ile ya mchina ilikuwa na tatizo la wafanyakazi walipofika mimi nilipigiwa simu na mchina akaniambia waandishi wamekuja, mimi nikapiga simu polisi nikaagiza wakawachukue waandishi wale niwakute polisi Oysterbay.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><span>\u201cNa huu utaratibu umewekwa na Serikali ya Wilaya ya Kinondoni, Mkuu wa Wilaya aliyekuwepo aliusimamia na huyu aliyepo sasa anausimamia. Lakini sasa kwa sababu nyie mlikuwa mnapita ndiyo mkaingia humo kununua bidhaa basi ni vizuri tuelewane kuwa siku nyingine kama mnataka kufanya lolote mje kwanza mueleze mnachotaka kufanya na mpate kibali ndiyo muendelee,\u201d alisema Ernest.<\/span><\/span><\/p>\n<p><span style=\"font-size:large;\"> <\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"font-size:large;\"><b><span>Tanzania PANORAMA INAENDELEA NA RIPOTI YA SAKATA HILI<\/span><\/b><\/span><span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span><span>\u00a0<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\">\u00a0<\/p>\n","protected":false},"excerpt":{"rendered":"<p>Richard Kayombo \u00a0 RIPOTA PANORAMA 0711 46 49 84 \u00a0 MAMLAKA ya Mapato (TRA) imetoa msimamo wa lugha zinazopaswa kutumika kwenye risiti zinazotolewa na mashine zote za kielekitroniki hapa nchni. Imesema risiti zote za kielekitroniki zinazotolewa kwa wateja zinatakiwa zitumie lugha rasmi ambazo ni Kiingereza na Kiswahili na si vinginevyo. Msimamo huo wa TRA umetolewa [&hellip;]<\/p>\n","protected":false},"author":1,"featured_media":0,"comment_status":"open","ping_status":"open","sticky":false,"template":"","format":"standard","meta":{"tdm_status":"","tdm_grid_status":"","_jetpack_memberships_contains_paid_content":false,"footnotes":"","jetpack_publicize_message":"","jetpack_publicize_feature_enabled":true,"jetpack_social_post_already_shared":false,"jetpack_social_options":{"image_generator_settings":{"template":"highway","default_image_id":0,"font":"","enabled":false},"version":2}},"categories":[1],"tags":[34],"coauthors":[],"class_list":{"0":"post-422","1":"post","2":"type-post","3":"status-publish","4":"format-standard","6":"category-uncategorized","7":"tag-habari"},"jetpack_publicize_connections":[],"jetpack_featured_media_url":"","jetpack_sharing_enabled":true,"jetpack_likes_enabled":true,"_links":{"self":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/422","targetHints":{"allow":["GET"]}}],"collection":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts"}],"about":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/types\/post"}],"author":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/users\/1"}],"replies":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcomments&post=422"}],"version-history":[{"count":0,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/422\/revisions"}],"wp:attachment":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fmedia&parent=422"}],"wp:term":[{"taxonomy":"category","embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcategories&post=422"},{"taxonomy":"post_tag","embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Ftags&post=422"},{"taxonomy":"author","embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcoauthors&post=422"}],"curies":[{"name":"wp","href":"https:\/\/api.w.org\/{rel}","templated":true}]}}