{"id":248,"date":"2022-06-02T10:10:00","date_gmt":"2022-06-02T10:10:00","guid":{"rendered":"https:\/\/msangirstz8.wordpress.com\/2022\/06\/02\/majaliwa-awapa-neno-wasaidizi-wake\/"},"modified":"2022-06-02T10:10:00","modified_gmt":"2022-06-02T10:10:00","slug":"majaliwa-awapa-neno-wasaidizi-wake","status":"publish","type":"post","link":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/?p=248","title":{"rendered":"MAJALIWA AWAPA NENO WASAIDIZI WAKE"},"content":{"rendered":"<p><span><\/span><\/p>\n<div style=\"text-align:center;\"><a href=\"https:\/\/blogger.googleusercontent.com\/img\/b\/R29vZ2xl\/AVvXsEjwUK3kHjhjyAP9McOAx_NSbIzunkfnXIp4UHp3fd5NzeMc1Waw-6Luga0tBttsdXjyET71pjSs_kHBf21jCozG-r8F0Afj4mE5ZBnaxyoOCox-oqZG2f29v2iqCGQ5C3SDpH8YETMvYq3fZN_HSpDUTHJAJ5uCQD8dBoO-nZthhbe1BH945LSK03TOeQ\/s750\/pm%201.jpeg\"><img loading=\"lazy\" decoding=\"async\" border=\"0\" height=\"360\" src=\"https:\/\/blogger.googleusercontent.com\/img\/b\/R29vZ2xl\/AVvXsEjwUK3kHjhjyAP9McOAx_NSbIzunkfnXIp4UHp3fd5NzeMc1Waw-6Luga0tBttsdXjyET71pjSs_kHBf21jCozG-r8F0Afj4mE5ZBnaxyoOCox-oqZG2f29v2iqCGQ5C3SDpH8YETMvYq3fZN_HSpDUTHJAJ5uCQD8dBoO-nZthhbe1BH945LSK03TOeQ\/w640-h360\/pm%201.jpeg\" width=\"640\" \/><\/a><\/div>\n<p><span style=\"font-size:medium;\"><i><span>\u00a0\u00a0 \u00a0<\/span><span>\u00a0\u00a0 \u00a0<\/span><span>\u00a0\u00a0 \u00a0<\/span><span>\u00a0\u00a0 \u00a0<\/span><span>\u00a0\u00a0 \u00a0<\/span><span>\u00a0\u00a0 \u00a0<\/span><span>\u00a0\u00a0 \u00a0<\/span><span>\u00a0\u00a0 \u00a0<\/span><span>\u00a0\u00a0 \u00a0<\/span><span>\u00a0\u00a0 \u00a0<\/span><span>\u00a0\u00a0 \u00a0<\/span>Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa<\/i><\/span><\/p>\n<p><span><span style=\"font-size:medium;\">RIPOTA WA WAZIRI MKUU<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:normal;margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span><span style=\"font-size:medium;\">WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kusimamia na kuratibu kikamilifu miradi iliyoko kwenye mikoa, wilaya na halmashauri zilizo kwenye sekta wanazosimamia.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:normal;margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span><span style=\"font-size:medium;\">Agizo hilo alilitoa Mei, 31, 2022 jijini Dodoma katika kikao baina yake na\u00a0Waziri wa TAMISEMI, naibu mawaziri, katibu mkuu, naibu makatibu wakuu na wakurugenzi na wakuu wa taasisi za wizara hiyo.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:normal;margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span><span style=\"font-size:medium;\">\u201cNendeni mkasimamie uratibu wa miradi kwenye mikoa, wilaya na halmashauri. Tambueni miradi iliyoko ni mingapi, mingapi iko vizuri, mingapi inasuasua kisha toeni taarifa kwa katibu mkuu,\u201d alisema Waziri Mkuu Majaliwa.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:normal;margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span><span style=\"font-size:medium;\">Aidha, aliwapongeza kwa kusimamia vizuri miradi inayotekelezwa kwa fedha zilizotolewa chini ya mpango wa maendeleo kwa ustawi wa taifa na mapambano dhidi ya UVIKO-19 ambayo kwenye elimu ilichukua muda mfupi sana kukamilika.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:normal;margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span><span style=\"font-size:medium;\">\u201cKama tuliweza kusimamia miradi ya fecha za UVIKO-19 na kuikamilisha chini ya miezi mitatu, ni kwa nini sasa hivi tushindwe kufanya hivyo kwa miradi mingine? Kuna miradi ilianza kujengwa kabla fedha za UVIKO-19 hazijatolewa, lakini hadi sasa haijakamilika. Ni kwa nini hali iko hivyo? mkurugenzi jiulize, ulipopewa mradi, ulipaswa kuisha lini? waziri na naibu mawaziri simamieni hilo na mfanye tathmini,\u201d alisema.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:normal;margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span><span style=\"font-size:medium;\">Akizungumzia mgawanyo wa majukumu kwa wakurugenzi wa wizara na wakuu wa idara, Waziri Mkuu Majaliwa aliwataka wakae ofisini na kutoa maamuzi ili kazi nyingine zifanyike badala ya kuweka msisitizo kwenye safari.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:normal;margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span><span style=\"font-size:medium;\">\u201cKaeni ofisini na kufanya maamuzi, hizo safari wapeni wasaidizi wenu na wakirudi wawape mrejesho.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:normal;margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span><span style=\"font-size:medium;\">\u201cKatibu mkuu na naibu makatibu wakuu fuatilieni utendaji wa wakuu wa idara. Kuwe na utaratibu wa kuondoka, siyo mtu anatimka tu kwenda mkoani au wilayani,\u201d alisema.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:normal;margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span><span style=\"font-size:medium;\">Aliwahimiza waandae mipango yao ya kazi kwa kufuata Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020 ambayo imeainisha kila sekta na kutaja miradi inayotakiwa kusimamiwa kwenye mikoa, wilaya, halmashauri na kata nchini.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:normal;margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span><span style=\"font-size:medium;\">\u201cNilishaelekeza kila mkuu wa idara apate nakara ya Ilani ya CCM na awe nayo mezani kwake. Tunatakiwa tuipitie na tuainishe mpango kazi kila mmoja kulingana na sekta yake,\u201d alisema.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:normal;margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span><span style=\"font-size:medium;\">Kuhusu matumizi ya fedha za umma, Waziri Mkuu Majaliwa alisema kwenye maeneo mengi alikopita amebaini kuwa matumizi ya fedha siyo mazuri na akasisitiza wasimamie eneo hilo ili kupata thamani halisi ya fedha kwenye miradi inayotekelezwa na Serikali.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:normal;margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span><span style=\"font-size:medium;\">Aliwataka wajiepushe na tamaa ya kutaka kuhusika kwenye manunuzi ya vifaa vya miradi hiyo.\u00a0<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:normal;margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span><span style=\"font-size:medium;\">\u201cTuna kamati za ujenzi katika kila kata. Iweje wao wafanye manunuzi wakati kamati zipo na zinasimamia? Wakuu wa idara mjiondoe kwenye nafasi ya kutuhumiwa. Hebu cheki kanuni zenu kuhusu kamati za ujenzi na masuala ya manunuzi zinasemaje,&#8221; alisema Waziri Mkuu Majaliwa.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:normal;margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span>\u00a0<\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:normal;margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span>\u00a0<\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:normal;margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span>\u00a0<\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span>\u00a0<\/span><\/p>\n","protected":false},"excerpt":{"rendered":"<p>\u00a0\u00a0 \u00a0\u00a0\u00a0 \u00a0\u00a0\u00a0 \u00a0\u00a0\u00a0 \u00a0\u00a0\u00a0 \u00a0\u00a0\u00a0 \u00a0\u00a0\u00a0 \u00a0\u00a0\u00a0 \u00a0\u00a0\u00a0 \u00a0\u00a0\u00a0 \u00a0\u00a0\u00a0 \u00a0Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa RIPOTA WA WAZIRI MKUU WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kusimamia na kuratibu kikamilifu miradi iliyoko kwenye mikoa, wilaya na halmashauri zilizo kwenye sekta wanazosimamia. Agizo hilo alilitoa [&hellip;]<\/p>\n","protected":false},"author":1,"featured_media":0,"comment_status":"open","ping_status":"open","sticky":false,"template":"","format":"standard","meta":{"tdm_status":"","tdm_grid_status":"","footnotes":""},"categories":[1],"tags":[34],"coauthors":[],"class_list":{"0":"post-248","1":"post","2":"type-post","3":"status-publish","4":"format-standard","6":"category-uncategorized","7":"tag-habari"},"_links":{"self":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/248","targetHints":{"allow":["GET"]}}],"collection":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts"}],"about":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/types\/post"}],"author":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/users\/1"}],"replies":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcomments&post=248"}],"version-history":[{"count":0,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/248\/revisions"}],"wp:attachment":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fmedia&parent=248"}],"wp:term":[{"taxonomy":"category","embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcategories&post=248"},{"taxonomy":"post_tag","embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Ftags&post=248"},{"taxonomy":"author","embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcoauthors&post=248"}],"curies":[{"name":"wp","href":"https:\/\/api.w.org\/{rel}","templated":true}]}}