{"id":2052,"date":"2021-03-28T21:48:00","date_gmt":"2021-03-28T21:48:00","guid":{"rendered":"https:\/\/msangirstz8.wordpress.com\/2021\/03\/28\/safari-ya-maisha-ya-kiroho-ya-dk-john-pombe-magufuli\/"},"modified":"2021-03-28T21:48:00","modified_gmt":"2021-03-28T21:48:00","slug":"safari-ya-maisha-ya-kiroho-ya-dk-john-pombe-magufuli","status":"publish","type":"post","link":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/?p=2052","title":{"rendered":"SAFARI YA MAISHA YA KIROHO YA DK. JOHN POMBE MAGUFULI"},"content":{"rendered":"<p>\u00a0<\/p>\n<table align=\"center\" cellpadding=\"0\" cellspacing=\"0\" class=\"tr-caption-container\" style=\"margin-left:auto;margin-right:auto;\">\n<tbody>\n<tr>\n<td style=\"text-align:center;\"><a href=\"https:\/\/i0.wp.com\/tanzaniapanorama.co.tz\/wp-content\/uploads\/2022\/11\/bdfd7-misa.jpg?ssl=1\" style=\"margin-left:auto;margin-right:auto;\" target=\"_blank\" rel=\"noopener\"><img data-recalc-dims=\"1\" loading=\"lazy\" decoding=\"async\" border=\"0\" height=\"266\" src=\"https:\/\/i0.wp.com\/tanzaniapanorama.co.tz\/wp-content\/uploads\/2022\/11\/bdfd7-misa.jpg?resize=400%2C266&#038;ssl=1\" width=\"400\" \/><\/a><\/td>\n<\/tr>\n<tr>\n<td class=\"tr-caption\" style=\"text-align:center;\">Maaskofu, Mapadre na Mashemasi wakiwa katika misa ya kumuombea Hayati Rais Dk. John Magufuli iliyofanyika Uwanja wa Magufuli, Chato mkoani Geita<\/td>\n<\/tr>\n<\/tbody>\n<\/table>\n<p><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"line-height:34.5pt;margin-bottom:18.75pt;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">NA PADRE RICHARD A. MJIGWA &#8211; C.PP.S \u2013 VATICAN<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">MAANA ya Kikristo ya kifo imefunuliwa katika mwanga wa fumbo la Pasaka, yaani mateso, kifo na ufufuko wa Kristo Yesu ambaye ndani yake mna tumaini la Wakristo.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Mkristo anayekufa katika Kristo huuacha mwili ili kwenda kukaa pamoja na Mwenyezi Mungu, milele yote.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Kwa Mkristo, siku ya kifo huanzia mwishoni mwa maisha yake ya Kisakramenti, utimilifu wa kuzaliwa kwake upya kulikoanzishwa na Sakramenti ya Ubatizo, kufanana kamili na sura ya mwana, kulikotolewa kwa mpako wa Roho Mtakatifu na ushirika katika karamu ya ufalme uliotangulizwa katika Ekaristi, hata kama ana lazima bado kutakaswa zaidi ili kuvikwa vazi la harusi!<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Askofu Mkuu, Protase Rugambwa, Katibu wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa watu, jumamosi tarehe 20 Machi 2021, kwa kushirikiana na ubalozi na wawakilishi wa Watanzania wanaoishi nchini Italia, ameongoza ibada ya misa takatifu kwa ajili ya kumkumbuka na kumwombea Hayati Dk. John Pombe Magufuli wa Tanzania aliyefariki dunia Machi 17, 2021.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"font-size:large;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\">Baada ya ibada ya misa, ilifuatia dua iliyoongozwa na Bwana Abdul Hamid Ahmed na mwishoni, Balozi George Kahema Madafa<\/span><b style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\">\u00a0<\/b><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\">alitoa neno la shukrani kwa wote waliohudhuria licha ya changamoto kubwa zinazotokana na janga la Virusi vya Korona, UVIKO-19.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"font-size:large;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\">Taarifa ya familia ya Hayati Dk. Magufuli, aliyefariki dunia Machi 17 ,2021<\/span><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\">\u00a0akiwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Emilio Mzena inasema kwamba, Dk. Magufuli alijiandaa kikamilifu kwa safari yake ya kiroho.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Kwa mpako mtakatifu wa wagonjwa na sala za makuhani, kanisa lote huwakabidhi wagonjwa kwa bwana aliyeteswa na kutukuzwa ili awainue na kuwaokoa.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><\/p>\n<table align=\"center\" cellpadding=\"0\" cellspacing=\"0\" class=\"tr-caption-container\" style=\"margin-left:auto;margin-right:auto;\">\n<tbody>\n<tr>\n<td style=\"text-align:center;\"><a href=\"https:\/\/i0.wp.com\/tanzaniapanorama.co.tz\/wp-content\/uploads\/2022\/11\/daf8a-misa2b2.jpg?ssl=1\" style=\"margin-left:auto;margin-right:auto;\" target=\"_blank\" rel=\"noopener\"><img data-recalc-dims=\"1\" loading=\"lazy\" decoding=\"async\" border=\"0\" height=\"225\" src=\"https:\/\/i0.wp.com\/tanzaniapanorama.co.tz\/wp-content\/uploads\/2022\/11\/daf8a-misa2b2.jpg?resize=400%2C225&#038;ssl=1\" width=\"400\" \/><\/a><\/td>\n<\/tr>\n<tr>\n<td class=\"tr-caption\" style=\"text-align:center;\">Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa katika misa ya kumuombea Hayati Rais Dk. John Magufuli iliyofanyika katika Uwanja wa Magufuli Chato mkoani Geita<\/td>\n<\/tr>\n<\/tbody>\n<\/table>\n<p><span style=\"font-size:large;\"><br \/><\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Na kwa hakika linawahimiza wajiunge kwa hiari na mateso na kifo cha Kristo Yesu ili kutoa mchango wao kwa manufaa ya Taifa la Mungu.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Akiwa katika hatari ya kifo, Dk. Magufuli alijiandaa kiroho kwa kupata mpako wa wagonjwa unaowajaza waamini nguvu ya Roho Mtakatifu. Huwaondoa katika enzi ya dhambi na kuwaweka huru.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Kwa wema wake usiokuwa na mipaka, Mwenyezi Mungu huwakirimia pia nafuu katika mateso yao na kuwajalia neema.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Msemaji wa familia ya Dk. Magufuli aliwaambia waombolezaji kwamba, kabla ya kifo chake alibahatika kupata huduma ya maisha ya kiroho iliyomwongezea amani na utulivu wa ndani na hivyo kujiandaa kupokea kifo chema!<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Familia ya Mungu Parokia ya Mtakatifu Petro, Jimbo Kuu la Dar es Salaam ilipata nafasi ya kumwombea na kumuaga muumini mwenzao waliyeshirikiana katika maadhimisho ya mafumbo ya kanisa<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Hapa pakawa ni mahali pa kanisa kutoa katekesi ya maana ya kuwakumbuka na kuwaombea marehemu kadiri ya mafundisho ya Kanisa Katoliki.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><\/p>\n<table align=\"center\" cellpadding=\"0\" cellspacing=\"0\" class=\"tr-caption-container\" style=\"margin-left:auto;margin-right:auto;\">\n<tbody>\n<tr>\n<td style=\"text-align:center;\"><a href=\"https:\/\/i0.wp.com\/tanzaniapanorama.co.tz\/wp-content\/uploads\/2022\/11\/9fffb-misa2b3.jpg?ssl=1\" style=\"margin-left:auto;margin-right:auto;\" target=\"_blank\" rel=\"noopener\"><img data-recalc-dims=\"1\" loading=\"lazy\" decoding=\"async\" border=\"0\" height=\"225\" src=\"https:\/\/i0.wp.com\/tanzaniapanorama.co.tz\/wp-content\/uploads\/2022\/11\/9fffb-misa2b3.jpg?resize=400%2C225&#038;ssl=1\" width=\"400\" \/><\/a><\/td>\n<\/tr>\n<tr>\n<td class=\"tr-caption\" style=\"text-align:center;\">Viongozi wa Serikali na waombolezi wakiwa katika misa ya kumuombea Hayati Rais Dk. John Magufuli kwenye Uwanja wa Magufiuli Chato mkoani Geita<\/td>\n<\/tr>\n<\/tbody>\n<\/table>\n<p><span style=\"font-size:large;\"><br \/><\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Askofu Mkuu, Yuda Thadaeus Ruwa&#8217;ichi, katika ibada ya misa takatifu kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, tarehe 20 Machi 2021 aliwaalika watu wa Mungu ndani na nje ya Jimbo Kuu la Dar es Salaam kuupokea msiba huu mzito kwa imani na matumaini kwa Kristo Yesu.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Hayati Dk. Magufuli katika uhai wake alimwamini Mwenyezi Mungu, akamfuata, akamshuhudia kwa vitendo na kumtumikia.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Roho za wenye haki ziko mikononi mwa Mwenyezi Mungu. Mtu mwenye haki, yuko tayari kumpatia Mungu masitahiki yake kwa kumwamini, kumwabudu na kumtumikia kwa imani.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Mtu mwenye haki anatoa stahiki kwa jirani zake kwa kuwapenda, kuwahurumia, kuwasaidia na kushikamana nao. Katika nafsi ya mtu mwenye haki, hujitunza, hujiheshimu na kuwajibika kikamilifu.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"font-size:large;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\">Ni katika muktadha huu, Hayati Dk. Magufuli, mtu wa haki anastahili kukumbukwa na kuombewa ili Mwenyezi Mungu mwingi wa huruma, msamaha na mapendo,<\/span><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\">\u00a0aweze kumsamehe dhambi na mapungufu yake ya kibinadamu, apende kuyaangalia majitoleo yake na hatimaye amkirimie maisha na uzima wa milele.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Dk. Magufuli aliunganishwa na kuzamishwa katika mateso, kifo na ufufuko wa Kristo Yesu kwa njia ya Sakramenti ya Ubatizo. Akawa ndugu yake Kristo na kufanyika kuwa Hekalu la Roho Mtakatifu.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Mama Kanisa, anamuombea ili Kristo mshindi aweze kumshirikisha katika ushindi wake kwa kumfufua siku ya mwisho na hatimaye kumkirimia maisha na uzima wa milele pamoja na watakatifu wake mbinguni.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Mama Kanisa katika huruma na upendo wake kwa ajili ya watoto wake waliotangulia katika usingizi wa amani wakiwa na tumaini la ufufuko wa wafu na uzima wa milele anawashukuru, anawakumbuka na kuwaombea.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"font-size:large;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\">Askofu Mkuu Protase Rugambwa, Katibu wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa watu katika mahubiri yake, amegusia kuhusu mahusiano na mafungamano kati ya muumini na Mwenyezi<b>\u00a0<\/b><\/span><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\">Mungu na kati ya muumini na jirani zake.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Kila mtu ni zawadi ya Mungu inayopaswa kupokelewa kwa moyo wa shukrani. Kuwaombea marehemu ni wajibu kwa waamini wote.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Askofu Mkuu ametumia fursa hii kutoa pole kwa Watanzania wote katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo. Anawaalika waamini pamoja na watu wote wenye mapenzi mema, kuendelea kuliombea Taifa la Tanzania bila kumsamahu Mama Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><\/p>\n<table align=\"center\" cellpadding=\"0\" cellspacing=\"0\" class=\"tr-caption-container\" style=\"margin-left:auto;margin-right:auto;\">\n<tbody>\n<tr>\n<td style=\"text-align:center;\"><a href=\"https:\/\/i0.wp.com\/tanzaniapanorama.co.tz\/wp-content\/uploads\/2022\/11\/b59e6-misa2b4.jpg?ssl=1\" style=\"margin-left:auto;margin-right:auto;\" target=\"_blank\" rel=\"noopener\"><img data-recalc-dims=\"1\" loading=\"lazy\" decoding=\"async\" border=\"0\" height=\"225\" src=\"https:\/\/i0.wp.com\/tanzaniapanorama.co.tz\/wp-content\/uploads\/2022\/11\/b59e6-misa2b4.jpg?resize=400%2C225&#038;ssl=1\" width=\"400\" \/><\/a><\/td>\n<\/tr>\n<tr>\n<td class=\"tr-caption\" style=\"text-align:center;\">Rais Mstaafu, Dk. Jakaya Kikwete akiwa katika misa ya kumuombea Hayati Rais Dk. John Magufuli, Chato mkoani Geita\u00a0<\/td>\n<\/tr>\n<\/tbody>\n<\/table>\n<p><span style=\"font-size:large;\"><br \/><\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Katika mahubiri yake, Askofu Mkuu Protase Rugambwa, amewataka waamini kukuza na kudumisha mahusiano na mafungamano yao na Mwenyezi Mungu pamoja na jirani zao kwa sababu uwepo wa kila mmoja wao ni kwa kadiri ya mapenzi, huruma, uwezo na utashi wa Mwenyezi Mungu.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Ni huyu Mungu mwingi wa huruma na mapendo atakayempokea mja wake katika makao ya uzima wa milele baada ya kumaliza safari ya maisha yake hapa duniani na \u201ckukunja kilago\u201d tayari kukutana na Mwenyezi Mungu, Hakimu mwenye haki.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"font-size:large;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\">Watu wa Mungu nchini Tanzania wanamshukuru Mwenyezi Mungu kwa zawadi ya Dk. Magufuli aliyejisadaka bila ya kujibakiza kwa ajili ya ustawi, maendeleo na mafao ya Watanzania wengi.<\/span><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\">\u00a0<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Waumini wanamwombea Dk. Magufuli ili Mwenyezi Mungu mwingi wa huruma, rehema na mapendo aweze kumtakasa na kumsamehe dhambi zake ili hatimaye, aweze kumpokea kwenye maisha ya uzima wa milele na tuzo isiyokuwa na mwisho.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Hayati Dk. Magufuli alikuwa ni sehemu ya wabatizwa na watoto wateule wa Mungu. Kumbe, kama waamini wanalo jukumu la kumkumbuka na kumwombea katika kifungo hiki cha Sakramenti ya Ubatizo. Kwa sababu katika maisha yake, alimkiri na kumshuhudia Mwenyezi Mungu kwa maneno na matendo yake adili.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Kwa wema na majitoleo yake kwa familia ya Mungu nchini Tanzania anastahili tuzo ya maisha ya uzima wa milele. Ikumbukwe kwamba hii ni tuzo inayotolewa kwa watoto wapendwa wa Mungu waliojitahidi katika safari ya maisha yao hapa ulimwenguni kutambua na kutekeleza mapenzi ya Mungu.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Kama binadamu wanahimizwa kumkumbuka na kumwombea ili Mwenyezi Mungu apende kumsafisha na kumtakasa pale aliposhindwa kutekeleza mapenzi ya Mungu katika maisha yake na pale aliposhindwa kutokana na udhaifu wa kibinadamu kuonesha upendo kwa jirani zake.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"font-size:large;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\">Waamini na watu wote wenye mapenzi mema waendelee kumwombea Hayati Dk. Magufuli ili Mwenyezi Mungu kwa huruma yake isiyokuwa na kikomo, apende kumsafisha, kumtakasa na kumsamehe dhambi zake<\/span><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"> ili hatimaye, aweze kumpokea kwenye ufalme wake wa milele, akiwa safi na \u201cmweupe pe kama tui la nazi.\u201d<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Askofu Mkuu Protase Rugambwa anakazia kwa kusema, Watanzania wanapoendelea kutafakuri mema na mazuri aliyotenda Hayati Dk. Magufuli, kiasi cha kukirimiwa wingi wa neema na baraka iwe ni fursa pia ya kuchunguza dhamiri, kila mtu kadiri ya nafasi yake. Lengo ni kujiandaa kwa ajili ya kifo chema.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Huu ni muda wa kumuenzi Dk. Magufuli si kwa maneno matupu! Bali kuendeleza kwa ari na moyo mkuu yale yote mema na mazuri aliyotenda Dk. Magufuli kama Rais wa awamu ya tano kwa ajili ya ustawi, maendeleo na mafao ya Watanzania wengi kiroho na kimwili.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Hii ni fursa makini ya kumwombea Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na viongozi wote watakaoteuliwa kumsaidia kuwaongoza Watanzania wanapoanza kuandika ukurasa mpya wa historia ya Tanzania.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Wananchi wanahimizwa kutoa ushirikiano wa dhati kwa Rais na viongozi wenzake ili kuliendeleza Taifa la Tanzania liweze kudumu katika amani kwa kukuza na kudumisha misingi ya haki, ustawi na maendeleo ya Watanzania kiroho na kimwili ili Tanzania iweze kuwa ni nchi ya furaha, amani na mwanga wa matumaini kwa watu wote. Kila mtu ajitahidi kutenda mema yanayompendeza Mungu na jirani.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"font-size:large;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\">Hayati Dk. Magufuli alikwisha waonya Watanzania kamwe wasibaguane kutokana na makabila yao, itikadi zao za kisiasa wala imani zao.<\/span><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\">\u00a0Wote wajisikie kuwa ni Watanzania na kwamba tofauti zao msingi ni utajiri na amana ya Watanzania wote.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Ndiyo maana Dk. Magufuli hakusita kuchangisha fedha kutoka kwa waamini wa dini mbalimbali ili kuboresha nyumba za ibada hasa kuzunguka Ikulu ya Chamwino.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Ni kiongozi aliyeamini kuhusu majadiliano ya kidini na kiekumene kwa ajili ya ustawi, maendeleo na mafungamano ya Watanzania wote.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Ni katika muktadha huu, Bwana Abdul Hamid Ahmed, Mtanzania muumini wa dini ya Kiislam katika dua yake, amemwomba Mwenyezi Mungu amuweke mahali stahiki Dk. Magufuli kutokana na mema yote aliyotenda hapa duniani. Pale alipoteleza kama binadamu apate msamaha.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\" style=\"margin-bottom:0.0001pt;margin-bottom:0;\"><span style=\"font-size:large;\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\">Wakati huo huo, jumuiya za watawa wanaoishi na kufanya utume wao nchini Tanzania hivi karibuni wameadhimisha Ibada ya Misa Takatifu, wakimkumbuka na kumuombea Hayati Dk. Magufuli<b>\u00a0<\/b><\/span><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\">pamoja na kumtakia heri na baraka Mama Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Watawa wamemuomba Mwenyezi Mungu awafariji na kuwadumisha Watanzania katika imani, amani, upendo, mshikamano ari na moyo wa uzalendo. <\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Masista Wakarmeli Wamisionari wa Theresia wa Mtoto Yesu wanaendelea na sala maalumu kwa ajili ya kuiombea nchi ya Tanzania. <\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">Katika salamu zake za rambirambi, Sista Donatella Capello amewasihi Watanzania kuendelea kushikamana kwa dhati pamoja na kuendelea kujifunza mpango wa Mungu katika maisha yao kama Taifa.<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">\u00a0<\/span><\/span><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><b><span style=\"color:#373737;font-family:Garamond, serif;\"><span style=\"font-size:large;\">ANDISHI HILI NI KWA HISANI YA MTANDAO WA HABARI WA VATICAN<\/span><span style=\"font-size:26pt;\"><\/span><\/span><\/b><\/p>\n<p class=\"MsoNormal\"><span>\u00a0<\/span><\/p>\n","protected":false},"excerpt":{"rendered":"<p>\u00a0 Maaskofu, Mapadre na Mashemasi wakiwa katika misa ya kumuombea Hayati Rais Dk. John Magufuli iliyofanyika Uwanja wa Magufuli, Chato mkoani Geita NA PADRE RICHARD A. MJIGWA &#8211; C.PP.S \u2013 VATICAN MAANA ya Kikristo ya kifo imefunuliwa katika mwanga wa fumbo la Pasaka, yaani mateso, kifo na ufufuko wa Kristo Yesu ambaye ndani yake mna [&hellip;]<\/p>\n","protected":false},"author":1,"featured_media":0,"comment_status":"open","ping_status":"open","sticky":false,"template":"","format":"standard","meta":{"tdm_status":"","tdm_grid_status":"","_jetpack_memberships_contains_paid_content":false,"footnotes":"","jetpack_publicize_message":"","jetpack_publicize_feature_enabled":true,"jetpack_social_post_already_shared":false,"jetpack_social_options":{"image_generator_settings":{"template":"highway","default_image_id":0,"font":"","enabled":false},"version":2}},"categories":[1],"tags":[],"coauthors":[],"class_list":{"0":"post-2052","1":"post","2":"type-post","3":"status-publish","4":"format-standard","6":"category-uncategorized"},"jetpack_publicize_connections":[],"jetpack_featured_media_url":"","jetpack_sharing_enabled":true,"jetpack_likes_enabled":true,"_links":{"self":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/2052","targetHints":{"allow":["GET"]}}],"collection":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts"}],"about":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/types\/post"}],"author":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/users\/1"}],"replies":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcomments&post=2052"}],"version-history":[{"count":0,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/2052\/revisions"}],"wp:attachment":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fmedia&parent=2052"}],"wp:term":[{"taxonomy":"category","embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcategories&post=2052"},{"taxonomy":"post_tag","embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Ftags&post=2052"},{"taxonomy":"author","embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcoauthors&post=2052"}],"curies":[{"name":"wp","href":"https:\/\/api.w.org\/{rel}","templated":true}]}}