{"id":10539,"date":"2026-06-02T09:45:48","date_gmt":"2026-06-02T09:45:48","guid":{"rendered":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/?p=10539"},"modified":"2026-06-02T09:45:58","modified_gmt":"2026-06-02T09:45:58","slug":"sherehe-za-arsenal-zazua-virugu-london","status":"publish","type":"post","link":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/?p=10539","title":{"rendered":"SHEREHE ZA ARSENAL ZAZUA VIRUGU LONDON"},"content":{"rendered":"\n<p class=\"wp-block-paragraph\">Watu sita wamejeruhiwa kwa kuchomwa kisu na wengine 24 kukamatwa wakati wa sherehe za kusherehekea ubingwa wa Ligi Kuu ya England wa Arsenal F.C. kaskazini mwa London, tukio lililogeuka kuwa la vurugu licha ya shamrashamra kubwa za mashabiki.<\/p>\n\n\n\n<p class=\"wp-block-paragraph\">Kwa mujibu wa Polisi wa Jiji la London, mamia ya maelfu ya watu walijitokeza kusherehekea mafanikio ya klabu hiyo, huku zaidi ya maafisa 500 wa polisi wakipelekwa kuhakikisha usalama. Hata hivyo, hali ilibadilika baada ya kuzuka kwa matukio ya vurugu na mashambulizi katika maeneo mbalimbali ya mkusanyiko huo.<\/p>\n\n\n\n<p class=\"wp-block-paragraph\">Polisi wamesema kuwa kati ya watu waliojeruhiwa kwa kuchomwa kisu, wengi hawakupata majeraha makubwa, isipokuwa mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 20 na kitu ambaye alikimbizwa hospitalini akiwa katika hali mbaya na inayotishia maisha baada ya kushambuliwa eneo la Hornsey Road muda mfupi kabla ya saa 2:30 usiku. Hata hivyo, hali yake baadaye iliripotiwa kuimarika na sasa yuko katika hali thabiti.<\/p>\n\n\n\n<p class=\"wp-block-paragraph\">Katika matukio mengine, afisa mmoja wa polisi alijeruhiwa mkononi kwa kukatwa, huku mwingine akipigwa kichwani na vitu vilivyokuwa vikirushwa na baadhi ya watu waliokuwa kwenye shamrashamra hizo.<\/p>\n\n\n\n<p class=\"wp-block-paragraph\">Kati ya watu 24 waliokamatwa, polisi wamesema 10 wanashukiwa kuwashambulia maafisa wa polisi, 3 wanachunguzwa kwa makosa ya unyanyasaji wa kingono, na mmoja anashukiwa kusababisha majeraha makubwa katika shambulio lililosababisha jeraha la kichwa.<\/p>\n\n\n\n<p class=\"wp-block-paragraph\">Mamlaka zinaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha vurugu hizo na kuhakikisha usalama wa matukio ya aina hiyo yanayoambatana na mikusanyiko mikubwa ya mashabiki.<\/p>\n","protected":false},"excerpt":{"rendered":"<p>Watu sita wamejeruhiwa kwa kuchomwa kisu na wengine 24 kukamatwa wakati wa sherehe za kusherehekea ubingwa wa Ligi Kuu ya England wa Arsenal F.C. kaskazini mwa London, tukio lililogeuka kuwa la vurugu licha ya shamrashamra kubwa za mashabiki. Kwa mujibu wa Polisi wa Jiji la London, mamia ya maelfu ya watu walijitokeza kusherehekea mafanikio ya [&hellip;]<\/p>\n","protected":false},"author":1,"featured_media":10540,"comment_status":"open","ping_status":"open","sticky":false,"template":"","format":"standard","meta":{"tdm_status":"","tdm_grid_status":"","_jetpack_memberships_contains_paid_content":false,"footnotes":"","jetpack_publicize_message":"","jetpack_publicize_feature_enabled":true,"jetpack_social_post_already_shared":true,"jetpack_social_options":{"image_generator_settings":{"template":"highway","default_image_id":0,"font":"","enabled":false},"version":2}},"categories":[215],"tags":[],"coauthors":[201],"class_list":["post-10539","post","type-post","status-publish","format-standard","has-post-thumbnail","category-michezo-kimataifa"],"jetpack_publicize_connections":[],"jetpack_featured_media_url":"https:\/\/i0.wp.com\/tanzaniapanorama.com\/wp-content\/uploads\/2026\/06\/ARSENAL.jpg?fit=557%2C359&ssl=1","jetpack_sharing_enabled":true,"jetpack_likes_enabled":true,"_links":{"self":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/10539","targetHints":{"allow":["GET"]}}],"collection":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts"}],"about":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/types\/post"}],"author":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/users\/1"}],"replies":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcomments&post=10539"}],"version-history":[{"count":1,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/10539\/revisions"}],"predecessor-version":[{"id":10541,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/10539\/revisions\/10541"}],"wp:featuredmedia":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/media\/10540"}],"wp:attachment":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fmedia&parent=10539"}],"wp:term":[{"taxonomy":"category","embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcategories&post=10539"},{"taxonomy":"post_tag","embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Ftags&post=10539"},{"taxonomy":"author","embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcoauthors&post=10539"}],"curies":[{"name":"wp","href":"https:\/\/api.w.org\/{rel}","templated":true}]}}