{"id":10485,"date":"2026-06-01T06:31:13","date_gmt":"2026-06-01T06:31:13","guid":{"rendered":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/?p=10485"},"modified":"2026-06-01T06:31:18","modified_gmt":"2026-06-01T06:31:18","slug":"iran-ya-shikilia-msimamo-dhidi-ya-marekani","status":"publish","type":"post","link":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/?p=10485","title":{"rendered":"IRAN YA SHIKILIA MSIMAMO DHIDI YA MAREKANI"},"content":{"rendered":"\n<p class=\"wp-block-paragraph\">Mkuu wa timu ya mazungumzo ya Iran na Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, amesema nchi yake haiiamini Marekani na haitakubali makubaliano yoyote ambayo hayatatoa dhamana ya kulinda haki na maslahi ya wananchi wa Iran.<\/p>\n\n\n\n<p class=\"wp-block-paragraph\">Akizungumza kupitia ujumbe wa video uliorushwa na televisheni ya taifa Jumapili, Ghalibaf alisema timu ya Iran itahakikisha masuala yote muhimu kwa taifa hilo yanazingatiwa kabla ya kusaini makubaliano yoyote na Washington.<\/p>\n\n\n\n<p class=\"wp-block-paragraph\">Kauli hiyo imekuja saa chache baada ya taarifa kuibuka kwamba Rais wa Marekani, Donald Trump, amewasilisha pendekezo jipya la mkataba wa amani kwa Iran lenye masharti makali zaidi, hatua inayodhihirisha kuwepo kwa tofauti kubwa kati ya pande hizo mbili.<\/p>\n\n\n\n<p class=\"wp-block-paragraph\">Mvutano huo unaweza kuchelewesha juhudi za kumaliza rasmi vita vilivyoanzishwa na Marekani na Israel dhidi ya Iran miezi mitatu iliyopita. Aidha, huenda ukachelewesha kufunguliwa tena kwa Mlango Bahari wa Hormuz, ambao Iran imeufunga kwa sababu za kiusalama tangu kuanza kwa mzozo huo.<\/p>\n\n\n\n<p class=\"wp-block-paragraph\">Kufungwa kwa njia hiyo muhimu ya baharini kumechangia kupanda kwa bei za mafuta katika soko la dunia, huku mataifa mbalimbali yakifuatilia kwa karibu maendeleo ya mazungumzo kati ya Tehran na Washington.<\/p>\n","protected":false},"excerpt":{"rendered":"<p>Mkuu wa timu ya mazungumzo ya Iran na Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, amesema nchi yake haiiamini Marekani na haitakubali makubaliano yoyote ambayo hayatatoa dhamana ya kulinda haki na maslahi ya wananchi wa Iran. Akizungumza kupitia ujumbe wa video uliorushwa na televisheni ya taifa Jumapili, Ghalibaf alisema timu ya Iran itahakikisha masuala [&hellip;]<\/p>\n","protected":false},"author":1,"featured_media":10486,"comment_status":"open","ping_status":"open","sticky":false,"template":"","format":"standard","meta":{"footnotes":""},"categories":[74],"tags":[],"coauthors":[201],"class_list":["post-10485","post","type-post","status-publish","format-standard","has-post-thumbnail","hentry","category-habari-kimataifa"],"amp_enabled":true,"jetpack_featured_media_url":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/wp-content\/uploads\/2026\/06\/IRAN.jpg","_links":{"self":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/10485","targetHints":{"allow":["GET"]}}],"collection":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts"}],"about":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/types\/post"}],"author":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/users\/1"}],"replies":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcomments&post=10485"}],"version-history":[{"count":1,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/10485\/revisions"}],"predecessor-version":[{"id":10487,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/posts\/10485\/revisions\/10487"}],"wp:featuredmedia":[{"embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=\/wp\/v2\/media\/10486"}],"wp:attachment":[{"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fmedia&parent=10485"}],"wp:term":[{"taxonomy":"category","embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcategories&post=10485"},{"taxonomy":"post_tag","embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Ftags&post=10485"},{"taxonomy":"author","embeddable":true,"href":"https:\/\/tanzaniapanorama.com\/index.php?rest_route=%2Fwp%2Fv2%2Fcoauthors&post=10485"}],"curies":[{"name":"wp","href":"https:\/\/api.w.org\/{rel}","templated":true}]}}