MAKOCHA WAITWA KUSOMEA UKOCHA

Date:

Share post:

MAKOCHA mbalimbali wa soka wametakiwa kujitokeza kushiriki kozi ya ukocha ngazi ya Diploma D, iliyopangwa kufanyika Julai 5 hadi 14, mwaka huu, wilayani Kigamboni, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na PANORAMA, mratibu wa mafunzo hayo, Issa Yahya, alisema milango ipo wazi kwa makocha waliosoma kozi ya ukocha ngazi ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF Grass root) .

Yahya alisema uthibitisho wa kushiriki mafunzo hayo utakwenda na washiriki kulipa ada Sh. 190,000.

” Maandalizi yanaendelea vizuri na tunaendelea kuhamasisha wadau kujitokeza kwa wingi kushiriki kozi kwa lengo la kupata elimu hii kwa manufaa ya Wilaya na Taifa kwa ujumla,” alisema Yahya.

Mratibu huyo alisema lengo la kozi hiyo ni kuzalisha makocha wengi na kuwaongezea ujuzi na maarifa ili waweze kwenda na wakati uliopo.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...

ISHU YA RASHFORD BADO PASUA KICHWA

MANCHESTER, UingerezaKOCHA wa Manchester United, Michael Carrick, amesema bado haijafahamika kama Marcus Rashford atarudi klabuni hapo au atabaki...

BARCA YAPATA MRITHI WA LEWANDOWSKI

CATALUNYA, HispaniaKLABU ya Barcelona imeanza mipango ya kumsajili mshambuliaji wa kati wa Real Mallorca, Vedat Muriqi, ikiamini anatosha...

ARSENAL AKILI YOTE KWA MONGA

LONDON, UingerezaARSENAL ya Kaskazini mwa Jiji la London imeonesha nia ya kumsajili winga anayefanya vizuri Ligi Daraja la...