CHALAMILA ATAKA KASI UPANUZI BARABARA YA UBUNGO – KIMARA

Date:

Share post:

ZERUBABEL CHUMA,

Dar es Salaam

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amemtaka mkandarasi anayefanya upanuzi wa barabara ya Morogoro, eneo la Ubungo Mataa hadi Kimara kuongeza kasi ya ujenzi.

Chalamila alitoa agizo hilo jana akiwa katika siku ya pili ya ziara ya kukagua miradi inayotekelezwa na serikali wilayani Ubungo, jijini Dar es Salaam.

Alisema mradi huo ni kiungo muhimu kwenye ukuaji wa uchumi hivyo ni budi ukamilike kwa wakati. Hivi sasa umefikia asilimia 45.

Akizungumza na wananchi wa eneo hilo, Chalamila alisema serikali imekwishaandaa mpango wa kupata magari ya kutosha ya mwendo kasi na kuwepo watoa huduma wengi badala ya mmoja, UDART.

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Lazaro Twange aliyeandamana na Chalamila kwenye ziara hiyo alisema, serikali inapanua barabara hiyo ili kupunguza msongamano wa magari.

Katika ziara hiyo, pia Chalamila alitembelea mradi wa Shule ya Msingi Msewe na Kituo cha Afya Makurumla.

MATUKIO KATIKA PICHA MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM, ALBERT CHALAMILA AKIKAGUA UPANUZI WA BARABARA YA UBUNGO ENEO LA UBUNGO – MATAA HADI KIMARA NA AKIZUNGUMZA NA WANANCHI.

About The Author

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

USIYOYAJUA KUHUSU KOCHA ALIYEANDIKA HISTORIA BUNDESLIGA

MUNICH, Ujerumani JINA la Marie-Louise Eta limeandika historia katika soka la Ujerumani baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa...

BURNA BOY HATAKI MAZOEA, ‘BIFU’ KWAKE KAWAIDA TU

HIVI karibuni, supastaa wa muziki wa Afrobeat, Burna Boy, aliingia kwenye mikono ya Chama cha 'Ma-dj' nchini Nigeria,...

BURKINA FASO IKO HOI AU HAI CHINI YA KAPTENI TRAORE?

HATUA ya kutangaza kuwa raia wake waaitarajie demokrasia imeibua maswali mengi juu ya uongozi wa Kapteni Ibrahim Traore...

SIMU YAKO CHANZO CHA UGONJWA WA MOYO, SARATANI?

UKWELI ulio wazi ni kwamba matumizi ya simu za mkononi yameongezeka kwa kasi duniani, Tanzania ikiwa na 'laini'...