MNEC SALIM ASAS KUFANYA ZIARA IRINGA 

Date:

Share post:

ANDREW CHALE

MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (MNEC – CCM) Mkoa wa Iringa Salim Abri Asas anatarajiwa kufanya ziara  maalum katika mkoa huo ambapo pia atakutana na Halmashauri Kuu za CCM Wilaya.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Katibu Siasa, Uenezi na Mafunzo Mkoa wa Iringa ziara hiyo inatarajia kuanzia Mufindi siku ya Jumamosi Agosti 3, mwaka huu.

“Tarehe 3 Agosti, 2024 Mufindi, Tarehe 4 Agosti, Kilolo, Tarehe 7 Agosti, Iringa Vijijini na mwisho atahitimisha tarehe 9 Agosti, Iringa mjini,” inasomeka taarifa hiyo.

Asas ameendelea kukiimarisha CCM katika Mkoa wa Iringa huku akiwa nguzo kwenye kushiriki miradi ya kimaendeleo kimkoa, Nyanda za Juu Kusini pamoja na Taifa kwa ujumla.

Pia anasifika kwa utendajikazi, ustamilivu, subra, busara, huruma na mapenzi yake kwa CCM na Taifa vimeendelea kumjengea taswira njema kwa wananchi.

Aidha, amekuwa mstari wa mbele kujitolea katika Sekta za Afya, Elimu, Miundombinu, mitaji ya wafanyabiashara wadogo (machinga), vijana na kinamama, lishe mashuleni, michezo na mengine mengi.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...

ISHU YA RASHFORD BADO PASUA KICHWA

MANCHESTER, UingerezaKOCHA wa Manchester United, Michael Carrick, amesema bado haijafahamika kama Marcus Rashford atarudi klabuni hapo au atabaki...

BARCA YAPATA MRITHI WA LEWANDOWSKI

CATALUNYA, HispaniaKLABU ya Barcelona imeanza mipango ya kumsajili mshambuliaji wa kati wa Real Mallorca, Vedat Muriqi, ikiamini anatosha...

ARSENAL AKILI YOTE KWA MONGA

LONDON, UingerezaARSENAL ya Kaskazini mwa Jiji la London imeonesha nia ya kumsajili winga anayefanya vizuri Ligi Daraja la...