WAZIRI MKUU MAJALIWA AMTEMBELEA LOWASSA HOSPITALINI

Date:

Share post:

RIPOTA WA WAZIRI MKUU

JOHANNESBURG, AFRIKA KUSINI

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesafiri kwenda Johannesburg, Afrika Kusini kumtembelea na kumjulia hali Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa ambaye amelazwa hospitalini nchini humo akipatiwa matibabu.

Waziri Mkuu Majaliwa amekwenda Afrika Kusini Disemba 28, 2022 kwa niaba ya Rais Samia Suluhu Hassan na sambamba na kumjulia hali Lowassa, amekutana na familia ya Lowassa na kuipatia salamu za pole kutoka kwa Rais Samia.

Akiwasilisha salamu za pole kutoka kwa Rais, Waziri Mkuu Majaliwa amesema Rais Samia anafuatilia mwenendo wa hali ya afya ya Lowassa kwa karibu na anamuombea afya njema.

Akizungumza baada ya kupokea salamu za Rais Samia, Mke wa Lowassa, Regina Lowassa alimshukuru Rais Samia kwa kuwa karibu na familia yake na kwa namna ambavyo anafuatilia matibabu ya mume wake.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

MAREKANI, CUBA: MZOZO MWINGINE UNAOSUBIRI KUITIKISA DUNIA

HAVANA, CubaRAIS wa Cuba, Miguel Diaz-Canel, hajaonesha unyonge, licha ya Taifa lake kuendelea kupewa presha kubwa na Rais...

LINDI YAIMARISHA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA WASH KUBORESHA AFYA ZA WANANCHI

Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zuwena Omary, amesema mkoa huo unaendelea kunufaika na utekelezaji wa afua...

WAZIRI MKUU AWASILI ARUSHA KWA ZIARA YAKE YA KIKAZI

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amewasili mkoani Arusha kwa ziara...

BARAZA LA MADIWANI MTAMA LAKUTANA, LAPONGEZA MAFANIKIO YA MIRADI YA MAENDELEO

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtama limefanya kikao chake cha robo ya tatu kwa mwaka...