LOLIONDO KULINDWA USIKU NA MCHANA,, MIPAKA YAKAMILIKA

Date:

Share post:

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitoa maelekezo kwa viongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii na Mkoa wa Arusha alipokuwa akikagua kazi ya uwekaji mipaka katika eneo la Loliondo, Ngorongoro jana.


●Vigingi 424 vyawekwa kama alama

●Barabara ya kilomita 108 yachongwa mpakani

●Kigingi namba moja maalumu kumkumbuka askari aliyepoteza maisha.

MWANDISHI MAALUM, LOLIONDO

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa jana alitangaza kukamilika kwa kazi ya uwekaji wa alama za mipaka katika Pori Tengefu la Loliondo, Ngorongoro mkoani Arusha.

Akizungumza jana baada ya kukagua eneo la Kilomita 1,500 zilizowekewa mipaka katika eneo la Ngorongoro, Waziri Mkuu Majaliwa alipongeza wote walioshiriki kufanya kazi ya kuweka mipaka na kuwataka wananchi kuepuka taarifa hasi na za upotoshaji kuhusu eneo hilo.

Alisema kazi hiyo imefanyika kwa nia njema ya kuhifadhi eneo hilo na hakuna mwananchi yoyote aliyehamishwa kwa nguvu katika eneo hilo.

“Eneo hili ni muhimu kwa kuwa lina vyanzo vya maji na mazalia ya nyumbu ambayo ni muhimu kwa uwepo wa maeneo ya Hifadhi za Serengeti na Ngorongoro,” alisema Majaliwa.

Waziri Mkuu Majaliwa alibainisha eneo la Ngoronforo litaendelea kulindwa wakati wote ili kuhifadhi eneo hilo ambalo ni muhimu kwa uhifadhi kitaifa na kimataifa.

Kwa upande wake, Waziri wa Maliasili na Utalii Pindi Chana alisema wizara na taasisi zilizo chini yake wataendelea kusimamia maeneo yote ya uhifadhi kwa niaba ya wananchi.

Mapema akimkaribisha Waziri Mkuu, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongella alisema kazi ya kuweka mipaka imekamilika kwa wakati na kwa mafanikio makubwa. Mongella ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa wa Arusha na msimamizi wa kazi hiyo, alisema Askari Garlus Mwita aliyepoteza maisha akiwa katika kazi ya kujenga mnara atapewa heshima kwa kigingi namba moja kupewa jina lake kama alama ya kumuenzi.

MATUKIO KATIKA PICHA ZIARA YA WAZIRI MKUU, KASSIM MAJALIWA ALIYOIFANYA JANA LOLIONDO, NGORONGORO


 

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...

ISHU YA RASHFORD BADO PASUA KICHWA

MANCHESTER, UingerezaKOCHA wa Manchester United, Michael Carrick, amesema bado haijafahamika kama Marcus Rashford atarudi klabuni hapo au atabaki...

BARCA YAPATA MRITHI WA LEWANDOWSKI

CATALUNYA, HispaniaKLABU ya Barcelona imeanza mipango ya kumsajili mshambuliaji wa kati wa Real Mallorca, Vedat Muriqi, ikiamini anatosha...

ARSENAL AKILI YOTE KWA MONGA

LONDON, UingerezaARSENAL ya Kaskazini mwa Jiji la London imeonesha nia ya kumsajili winga anayefanya vizuri Ligi Daraja la...