WAZIRI MAVUNDE AZINDUA MAFUNZO KWA VIJANA

Date:

Share post:


Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Ulemavu, Anthony Mavunde akizungumzawakati wa ufunguzi wa mafunzo ya utambuzi wa ujuzi uliopatikana nje ya mfumo rasmi
NAIBU Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Ulemavu, Anthony Mavunde amezindua mafunzo ya utambuzi wa ujuzi uliopatikana nje ya mfumo rasmi kwa vijana 847 wa mikoa ya Mtwara, Lindi, Morogoro, Pwani, na Dar es Salaam.
Akizindua mafunzo hayo mkoani Mtwara, Naibu Waziri Mvunde aliwataka vijana kuchangamkia fursa badala ya kusubiri serikali itoe matangazo, au kuwatafuta kwa ajili ya kuwapatia ujuzi. 
“Msingi wa maisha ya kijana unaanzia hapa, kijana wa kitanzania jiamini, timiza wajibu wako. Vijana mliopata fursa ya kuingia kwenye mafunzo haya itumie vizuri fursa hii. Muwe waaminifu na wawajibikaji.
“Acheni tamaa, tambueni kuwa ni kaburi peke yake watu huanza kuchimba toka juu kwenda chini lakini maisha yananzia chini kwenda juu,” alisema Naibu Waziri Mavunde.
Alisema mafunzo ya utambuzi wa ujuzi uliopatikana nje ya mfumo rasmi yanatolewa na serikali hivyo vijana  wahakikishe wanatumia vizuri fedha zinazotolewa katika mafunzo.
Tatarifa ya Kitengo cha Mawasiliano serikalini, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Ulemavu. 

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

KIFO CHA BOSI KINAVYOITESA LEICESTER CITY

LONDON, UingerezaMIAKA 10 iliyopita, Leicester City waliishangaza dunia walipotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England (EPL) mbele ya...

ISHU YA RASHFORD BADO PASUA KICHWA

MANCHESTER, UingerezaKOCHA wa Manchester United, Michael Carrick, amesema bado haijafahamika kama Marcus Rashford atarudi klabuni hapo au atabaki...

BARCA YAPATA MRITHI WA LEWANDOWSKI

CATALUNYA, HispaniaKLABU ya Barcelona imeanza mipango ya kumsajili mshambuliaji wa kati wa Real Mallorca, Vedat Muriqi, ikiamini anatosha...

ARSENAL AKILI YOTE KWA MONGA

LONDON, UingerezaARSENAL ya Kaskazini mwa Jiji la London imeonesha nia ya kumsajili winga anayefanya vizuri Ligi Daraja la...