ZIARA YA NAIBU WAZIRI WA MADINI, STANSLAUS NYONGO KATIKA MGODI WA HAMAD MINE SCALE ULIOPO WILAYA YA KWERWA, MKOA WA KAGERA
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (mwenye Kaunda Suti-
mbele) na Ujumbe wake, baada ya kukagua mitambo inayotumika
kusaga mawe yenye Madini ya Bati (kulia) katika Mgodi wa Hamad
Mine Scale, uliopo eneo la Omukasheni, Wilaya ya Kyerwa, Mkoa
wa Kagera, Februari 28 mwaka huu, akiwa katika ziara ya kazi.
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (katikati), akikagua
madini ghafi ya Bati (aliyoshika mkononi) na kuzungumza na
mmoja wa wamiliki wa mtambo wa kuchakata madini hayo, Hassan
Ibar (kushoto), alipotembelea na kuukagua mtambo huo
unaomilikiwa na Kampuni ya African Top Minerals, wilayani
Kyerwa, Mkoa wa Kagera.
Mmoja wa wamiliki wa mtambo wa kuchenjua Madini ya Bati wa
TanzaPlus Minerals, Salim Mhando (kushoto), akimuonyesha Naibu
Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (wa pili kutoka kushoto), moja
ya mashine zinazotumika kuchakata madini hayo. Naibu Waziri
alitembelea na kukagua mtambo huo uliopo Nyaluzumbulwa
wilayani Kyerwa, Mkoa wa Kagera
Madini ya Bati yaliyo ghafi.
Ujumbe wa Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo wakikagua
shimo linalochimbwa Madini ya Bati katika Mgodi wa Hamad Mine
Scale, uliopo eneo la Omukasheni, Wilaya ya Kyerwa mkoani
Kagera.











