Kiswahili chakwamisha kesi mahakakani

Date:

Share post:

ARUSHA
Mahakama ya Afrika Mashariki (EACJ) leo imeshindwa kusikiliza kesi iliyofunguliwa na Baraza la Serikali ya Kijiji cha Ololosokwan kwa sababu hati ya mashitaka imeandaliwa kwa Lugha ya Kiswahili.
Baraza la Serikali ya Kijiji cha Ololosokwan kilicho Wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha limefungua kesi dhidi ya Serikali ya Tanzania likiiomba EACJ iizuie Serikali kuwahamisha kwenye ardhi wanayoishi.
Shauri hilo liko mbele ya majaji watatu wa EACJ wakiongozwa na Jaji Kiongozi, Monica Mugenyi ambaye aliahirisha shauri hilo kwa maelezo kuwa hati ya mashtaka iliyowasilishwa mahakamani, kwenye kesi namba 15 ya mwaka 2017 ina kasoro kwa sababu imeandikwa kwa Kiswahili badala ya Kingereza ambacho kinatambulika mahakamani hapo.
Aidha, alisema hati zimesainiwa na mawakili wawili tofauti hivyo mahakama imeshindwa kujua itumie hati gani ya mashtaka.
“Hati hizi zimesainiwa na mawaikili wawili tofauti, hakuna hati ya kiapo inayoonyesha ni halali na imefuata taratibu za kimahakama. Lakini pia mmeandika kwa Lugha ya Kiswahili wakati mnajua mahakama hii inatumia Lugha ya Kingereza.
“Kutokana na kasoro hizo tunalazimika kuahirisha kesi hii hadi hapo mtakaporekebisha kasoro mbalimbali zilizopo kwenye hati ya kiapo,” alisema Jaji Mugenyi.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

EMERY APANGA KUIBOMOA BARCELONA

LONDON, Uingereza KOCHA wa Aston Villa, Unai Emery, anaitaka saini ya beki wa Barcelona, Alejandro Balde, na amewaambia mabosi...

BAYERN YAMKODOLEA MACHO KIUNGO WA TOTTENHAM

LONDON, Uingereza BAYERN Munich inampigia hesabu za karibu kiungo wa Tottenham na timu ya Taifa ya Senegal, Pape Matar...

RIPOTI: IDADI YA WAHAMIAJI ULAYA IMEVUNJA REKODI, UJERUMANI INAONGOZA

LONDON, UingerezaRIPOTI mpya imeonesha kuwa Ulaya nchi za Ulaya zlipokea wahamiaji milioni 64 mwaka 2025, likiwa ni ongezeko...

RAIS WA TAIWAN ASITISHA ZIARA YAKE AFRIKA, CHINA IKITAJWA KUWA CHANZO

TAIPEI, TaiwanRAIS wa Taiwan, Lai Ching-te, ameahirisha ziara yake nchini Eswatini, huku akiitaja China kuwa ndiyo chanzo cha...